Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari Mwili wa kada wa Chadema aliyefia vitani Ukraine wawasili, kuzikwa Mbeya
HabariHabari Mchanganyiko

Mwili wa kada wa Chadema aliyefia vitani Ukraine wawasili, kuzikwa Mbeya

Spread the love

MWILI wa Kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo-Chadema, aliyefia vitani nchini Ukraine akiipigania Urusi, Nemes Tarimo, umewasili nchini leo Ijumaa saa 10:25 alfajiri na kupokewa na ndugu katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Mwili huo ambao unadaiwa kuharibika vibaya kutokana na kukaa muda mrefu tangu marehemu afariki dunia tarehe 24 Oktoba 2022, umepelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili kuongezewa dawa ya kuhifadhi.

Kutokana na hali hiyo ndugu wameeleza kuwa mwili huo utaagwa nyumbani kwake Saranga jijini Dar es Salaam ambapo pia itafanyika Ibada ya misa na baadae mchana utaanza kusafirishwa kwenda mkoani Mbeya kwaajili ya maziko.

“Mwili ulishuka uwanja wa ndege majira ya saa 10:25 alfajiri na sisi tulikuwa pale, tunaishukuru sana Serikali imetuunga mkono na ilitusaidia katika kuupokea na kuweka mambo yote sawa na baada ya kukamilisha taratibu zote za pale airport, tukaona tuupeleke Muhimbili kwaajili ya kuweka sawa zaidi ili watu waweze kuuaga,” amesema amesema Henry Sandu ambaye ni msemaji wa familia kuhusu utaratibu wa mazishi.

Waombolezaji wameendelea kufika nyumbani kwa Tarimo jijini Dar es Salaam na miongoni mwa waliofika msibani hapo ni makada wenzake akiwemo Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika ambaye alisaini kitabu cha rambirambi na kisha kuondoka na imeelezwa kuwa anaweza kurejea kuaga mwili wa Tarimo

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!