Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mwigamba amsikitisha Zitto Kabwe
Habari za SiasaTangulizi

Mwigamba amsikitisha Zitto Kabwe

Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT-Wazalendo (kushoto) akiwa na Samson Mwigamba kabla hajajivua uanachama
Spread the love

ZITTO Kabwe, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, ameeleza masikitiko juu uongo uliotumiwa na walikuwa wafuasi wa chama hicho, Samson Mwigamba na wenzake kuwa chama hicho kimekiuka misingi iliyojiwekea, anaandika Faki Sosi.

Zitto ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kwenye Ofisi Kuu za Chama hicho ambapo amesema kuwa Mwigamba hajaweka wazi misingi ambayo chama hicho kimekiuka hatimaye akatangaza kutimka.

“Kutokana na unyeti wa madai haya, kikao cha Kamati ya Uongozi kiliitishwa na mtoa madai alipewa mwaliko ili aweze kufafanua jinsi misingi au msingi wa chama anaodhani umevunjwa,” amesema Zitto.

Zitto ameongeza: “Tulifanya hivi kwa sababu tangu kuasisiwa kwake, chama cha ACT-Wazalendo kimejipambanua kuwa chama kinachosimamia misingi.

“Licha ya kutumiwa mwaliko, mtoa madai hakuhudhuria kikao cha Kamati ya Uongozi na badala yake kuitisha mkutano na waandishi wa habari ambapo alitangaza kujiuzulu uanachama kwa madai ya kuunga mkono juhudi za serikali ya sasa.”

Zitto amesema kuwa chama hicho kimejitathmini na kujiona bado kipo kwenye misingi imara iliyojiwekea ya kiokombozi kwenye masuala mbalimbali ya kitaifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!