Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mwigamba amsikitisha Zitto Kabwe
Habari za SiasaTangulizi

Mwigamba amsikitisha Zitto Kabwe

Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT-Wazalendo (kushoto) akiwa na Samson Mwigamba kabla hajajivua uanachama
Spread the love

ZITTO Kabwe, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, ameeleza masikitiko juu uongo uliotumiwa na walikuwa wafuasi wa chama hicho, Samson Mwigamba na wenzake kuwa chama hicho kimekiuka misingi iliyojiwekea, anaandika Faki Sosi.

Zitto ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kwenye Ofisi Kuu za Chama hicho ambapo amesema kuwa Mwigamba hajaweka wazi misingi ambayo chama hicho kimekiuka hatimaye akatangaza kutimka.

“Kutokana na unyeti wa madai haya, kikao cha Kamati ya Uongozi kiliitishwa na mtoa madai alipewa mwaliko ili aweze kufafanua jinsi misingi au msingi wa chama anaodhani umevunjwa,” amesema Zitto.

Zitto ameongeza: “Tulifanya hivi kwa sababu tangu kuasisiwa kwake, chama cha ACT-Wazalendo kimejipambanua kuwa chama kinachosimamia misingi.

“Licha ya kutumiwa mwaliko, mtoa madai hakuhudhuria kikao cha Kamati ya Uongozi na badala yake kuitisha mkutano na waandishi wa habari ambapo alitangaza kujiuzulu uanachama kwa madai ya kuunga mkono juhudi za serikali ya sasa.”

Zitto amesema kuwa chama hicho kimejitathmini na kujiona bado kipo kwenye misingi imara iliyojiwekea ya kiokombozi kwenye masuala mbalimbali ya kitaifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!