Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mweusi akutwa kanyongwa California
Kimataifa

Mweusi akutwa kanyongwa California

Marehemu Robert Fuller
Spread the love

ROBERT Fuller (24), mmarekani mweusi amekutwa ananing’inia kwenye mti baada ya kunyongwa katika mji wa Palmdale, Califonia nchini Marekani. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Familia ya Robert imetaka maelezo kutoka kwa jeshi la polisi jijini humo kuhusu kifo cha ndugu yao. Kifo hicho kimebainika ikiwa ni siku mbili baada ya Rayshard Brooks (27) kupigwa risasi na polisi wa Atlanta na kuuawa, pia wiki tatu baada ya polisi wa Minnesota kumuua George Floyd (46).

Nchini humo, maandamano kupinga ubaguzi wa rangi yameendelea kushika kasi. Mwili wa Robert umebainika Jumamosi ya mwisho wa wiki. Taarifa za awali za polisi jijini humo zinadai, Robert anaweza kuwa amejinyonga mwenyewe.

Hata hivyo, polisi wamesema wanasubiri ripoti kamili. Familia ya Robert imehoji ‘anawezaje kujinyonga wakati hakuna mvutano wowote?’

“Kila wanachotueleza hakielekeani na ukweli wowote,” amesema dada yake Robert, Diamond Alexander ambaye ni miongoni mwa waandamanaji wanaopinga ubaguzi wa rangi kwenye maandamano yanayoendelea sasa nchi humo.

Amesema, wamekuwa wakipokea maelezo tofauti kutoka kwa polisi tofauti kuhusu kifo cha ndugu yao na kwamba, hawaamini kama Robert alijiua mwenyewe.

“Tumekuwa tukipokea majibu tofauti. Ukikutana na polisi mwingine anakupa jibu tofauti, sasa tunachotaka ni kujua ukweli. Kaka yangu hajajinyonga, hapana hakujinyonga,” amesema Diamond.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!