Friday , 9 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Mwandishi gazeti la Uhuru anusurika kifo kwa ajali
Habari Mchanganyiko

Mwandishi gazeti la Uhuru anusurika kifo kwa ajali

Gari la Mariam Mziwanda (katikati) lilivyobanwa na maroli mawili
Spread the love

MWANDISHI wa gazeti la Uhuru, Mariam Mziwanda amenusurika kifo katika ajali ya gari iliyotokea usiku huu maeneo ya Tabata jijini Dar es Salaam baada gari yake kugongwa na kubanwa na magari mawili. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Ajali hiyo imetokea majira ya saa 4:40 usiku huu maeneo ya TOT- Tabata baada ya gari lenye namba za usajiri T222 DJX alilokuwa akiendesha kufinywa na magari mawili na kukandamizwa na kontena.

Mariam baada ya ajali hiyo amekimbizwa katika hospitali ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu na Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea aliyefika eneo la ajali muda mfupi baada ya kutokea ajali hiyo.

Kwa mujibu wa Kubenea, alimkuta Mariam akiwa tayari ametoka katika ajali hiyo, akilalamika maumivu makali kifuani, hivyo kulazimika kumkimbiza hospitali kwa matibabu zaidi.

DWqzKNfX4AAgqlL

DWqzZL1X4AAN3E1

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi zaidi ya 100 wapigwa msasa wa udereva kukabiliana na ajali

Spread the love  KATIKA kuhakikisha wimbi la ajali za barabarani zinapungua kama...

Habari MchanganyikoTangulizi

Serikali yakana kuhamisha kwa nguvu jamii ya Kimasai Loliondo

Spread the loveWAZIRI wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, Dk. Damas Ndumbaro,...

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

error: Content is protected !!