MTOTO wa Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, Muhoozi Kainerugaba amezua mjadala mpya nchini Uganda kwa kudai kuwa ndiye rais anayefuata wa nchi hiyo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Muhoozi alionyesha imani kuwa upinzani chini ya mwanamuziki aliyegeukia siasa Robert Kyagulanyi ‘Bobi Wine’ hautafua dafu kuongoza nchi baada ya kustaafu kwa baba yake.
“Kwa upinzani wa Uganda, baada ya baba yangu, nitawashinda vibaya katika uchaguzi wowote. Waganda wananipenda zaidi kuliko watakavyowahi kuwapenda,” alisema kupitia Twitter tarehe 14 Oktoba, 2022.
Uganda inatarajiwa kufanya uchaguzi mkuu mwaka wa 2026 kumchagua rais mpya. Museveni ameiongoza nchi hiyo tangu alipoingia madarakani mwaka 1978.
Aidha, Bobi Wine ambaye ni kiongozi wa chama cha upinzani cha National Unity Platform, alitangaza azma yake ya urais kwa mara ya kwanza mwaka wa 2019 lakini akashindwa na Museveni katika uchaguzi wa 2021.
To the Ugandan opposition, after my father, I will defeat you badly in any election. Ugandans love me more than they'll ever love you.
— Muhoozi Kainerugaba (@mkainerugaba) October 14, 2022
Hii si mara ya kwanza kwa Muhoozi kutoa maoni kuhusu mrithi wa urais kwani Mei 2019, Muhoozi alichapisha ‘meme’ inayoonyesha jinsi yeye na ‘kaka yake’ walivyokuwa waking’ang’ania nafasi hiyo.
Aliandika, “Mimi na kaka yangu mdogo Kabobi tukibishana kuhusu nani anaweza kujaza viatu vya baba yangu! Shukrani kwa msanii bora nchini Uganda.”
Akijibu tweet hiyo Bobi Wine alisema mimi sio kaka yako na wala sishindani na viatu vya baba yako, unastahili viatu vya M7, ng’ombe wake na hata kofia yake, kosa moja unalofanya ni kudhani Uganda ndio moja ya mali za baba yako ili urithi.”
Kiongozi huyo wa upinzani siku za nyuma alidai kuwa Museveni alikuwa akimtayarisha Muhoozi kuwania kiti hicho.
Leave a comment