Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mwanaye Museveni agomea magizo ya baba yake
Kimataifa

Mwanaye Museveni agomea magizo ya baba yake

Spread the love

 

SIKU moja baada ya Rais wa Uganda, Yoweri Museveni kuweka wazi kwamba atamlazimisha mwanaye Muhoozi Kainerugaba ambaye pia ni jenerali mkuu wa majeshi ya Uganda kwamba aache kutumia mtandao wa Twitter, Muhoozi ameibuka na kudai kwamba hang’atuki ng’o katika mtandao huo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Muhoozi kupitia kwenye mtandao huo wa Twitter amejibu madai hayo na kusema kwamba hamna mtu yeyote atakayemlazimisha kufanya jambo lolote kwa sababu yeye pia ni mtu mzima.

Jenerali huyo wa jeshi ambaye hivi karibuni ameibua mijadala kutokana na jumbe zake anaoziweka katika mtandao huo wa twitter, amesisitiza kuwa mtu mzima ambaye hawezi kupigwa marufuku kufanya chochote.

“Nasikia mwanahabari fulani kutoka Kenya alimwomba baba’ngu anipige marufuku kutoka kwa Twitter? Je, huo ni utani fulani? Mimi ni mtu mzima na hakuna mtu atakayenipiga marufuku kwa lolote!” aliandika.

Museveni ambaye alikuwa katika mahojiano ya kipekee na mwanahabari wa Kenya, Sophia Wanuna alisema kwamba mtandao wa Twitter si mbaya bali kinachozingatiwa ni kile ambacho mtu anapakia kwenye akaunti yake.

“Unatarajia kumwambia Muhoozi atoke Twitter pengine?” Wanuna alimuuliza Rais Museveni ambaye alijibu;

“Jenerali Muhoozi ataondoka Twitter. Tumekuwa na mjadala huu, unajua Twitter sasa hivi ni njia ya kisasa ya kuwasiliana na yeye ameungana na vijana wenzake ambao anafanya mambo nao, lakini suala ni kuhusu ni kile unachotweet,” Museveni alijibu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!