Saturday , 2 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Mwanamuziki apiga gitaa wakati wa upasuaji
Kimataifa

Mwanamuziki apiga gitaa wakati wa upasuaji

Gitaa
Spread the love

MWANAMUZIKI nchini India apiga gitaa kwenye meza ya kufanyia upasuaji ili kuwasaidia madaktari kutibu mishipa (involuntary muscle spasms) katika vidole vyake, anaandika Jovina Patrick.

Abhishek Parasad aliombwa na madakdari kupiga gitaa kila wakati walipokuwa wanatibu tatizo hilo linalojulikana kama “musician’s dystonia” katika ubongo wake.

Tatizo hilo katika mishipa ya Prasad ilimzuia kutumia vidole vyake, katika mkono wake wa  kushoto wakati akipiga gitaa.

Prasad mwanzo alidhani tatizo hilo linasababishwa na mazoezi ya mara kwa mara ya kupiga gitaa. Akajaribu kupumzika kwa muda lakini alipoanza kupiga gitaa hali ikawa vile vile.

Prasad anasema,“Baadhi ya madaktari waliniambia ni matatizo madogo tu katika mishipa, nikikapewa dawa za kutuliza maumivu, lakini hali haikubadilika.”

Daktari Shahara Srinivasan alimshauri kufanya upasuaji mara baada ya kugundua ana tatizo la “musician dystonia” na kumtoa hofu kuwa itakuwa sawa.”nilishauriwa kufanya upasuaji wa ubongo lakini nilikuwa mwoga sana. Daktari Shahara Srinivasan alinitia moyo” alisema Prasad.

Anasema baada ya upasuaji wiki moja baadaye vidole vyake vilifunguka na kurudi katika hali ya kawaida.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

Kimataifa

Mateka wa Israel, Gaza kuanza kuachiwa leo

Spread the loveMakubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Israel na vikosi vya...

Kimataifa

Israel, Hamas kusitisha mapigano kwa muda

Spread the loveNCHI ya Israel, pamoja na kikundi cha wanamgambo wa kiislamu,...

error: Content is protected !!