Thursday , 18 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mwanamuziki apiga gitaa wakati wa upasuaji
Kimataifa

Mwanamuziki apiga gitaa wakati wa upasuaji

Gitaa
Spread the love

MWANAMUZIKI nchini India apiga gitaa kwenye meza ya kufanyia upasuaji ili kuwasaidia madaktari kutibu mishipa (involuntary muscle spasms) katika vidole vyake, anaandika Jovina Patrick.

Abhishek Parasad aliombwa na madakdari kupiga gitaa kila wakati walipokuwa wanatibu tatizo hilo linalojulikana kama “musician’s dystonia” katika ubongo wake.

Tatizo hilo katika mishipa ya Prasad ilimzuia kutumia vidole vyake, katika mkono wake wa  kushoto wakati akipiga gitaa.

Prasad mwanzo alidhani tatizo hilo linasababishwa na mazoezi ya mara kwa mara ya kupiga gitaa. Akajaribu kupumzika kwa muda lakini alipoanza kupiga gitaa hali ikawa vile vile.

Prasad anasema,“Baadhi ya madaktari waliniambia ni matatizo madogo tu katika mishipa, nikikapewa dawa za kutuliza maumivu, lakini hali haikubadilika.”

Daktari Shahara Srinivasan alimshauri kufanya upasuaji mara baada ya kugundua ana tatizo la “musician dystonia” na kumtoa hofu kuwa itakuwa sawa.”nilishauriwa kufanya upasuaji wa ubongo lakini nilikuwa mwoga sana. Daktari Shahara Srinivasan alinitia moyo” alisema Prasad.

Anasema baada ya upasuaji wiki moja baadaye vidole vyake vilifunguka na kurudi katika hali ya kawaida.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!