Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mwanamke wa kwanza ajitosa urais Zanzibar
Habari za Siasa

Mwanamke wa kwanza ajitosa urais Zanzibar

Mwantum Mussa Sultan akiwa na fomu za kuwania Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Spread the love

MWANTUM Mussa Sultan, amekuwa mwanamke wa kwanza kujitosa katika mchakato wa kuomba kuteuliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM), kugombea Urais wa Zanzibar. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Mwantuma amechukua fomu Leo Ijumaa tarehe 19 Juni 2020 katika Ofisi za CCM visiwani Zanzibar zilizoko Kisiwandui na kukabidhiwa Cassian Gallo’s, katibu wa Kamati Maalumu ya NEC Idara ya Oganaizesheni Zanzibar.

Mara baada ya kukabidhiwa, Mwantumu amesema, amefanya hivyo ili kutoa hamasa kwa wanawake kujitosa katika kinyang’anyiro hicho, kutimiza sera ya haki sawa kwa wote.

“Nimekuja kuwapa hamasa kina mama wenzangu ili na sisi wanawake tujitokeze. Tuko wengi bila wanawake hakuna kitu, tujitokeze kuchukua fomu tupate asilimia yetu tuliyoomba ya hamsini hamsini,” amesema Mwantumu.

Mwantumu anakuwa kada wa 11 wa CCM kujitosa katika kinyang’anyiro hicho, tangu zoezi hilo la siku 15 lifunguliwe Jumatatu ya tarehe 15 Juni 2020.

Zoezi hilo linaloenda sambamba na utafutaji wadhamini 250 kwa kila mgombea, linatarajiwa kufika tamati tarehe 30 Juni mwaka huu.

Mwantuma amechukua fomu akitanguliwa na Waziri wa Maji, Profesa Makama Mbarawa.

Wengine waliokwisha chukua fomu ni; Mbwana Bakari Juma alikuwa mtu wa kwanza kufungua dimba hilo.

Balozi Ali Abeid Karume ambaye ni mtoto wa Rais wa kwanza wa Zanzibar, Hayati Abei Aman Karume kisha akafuatiwa na Mbwana Yahaya Mussa ambaye mpaka sasa ndiye mwanachama kijana aliyejitosa kuchukua fomu.

Mtaalamu wa uchumi aliyewahi kushika nafasi mbalimbali za uongozi katika tawala zilizipita visiwani Zanzibar, Omary Sheha Mussa alikuwa wan ne kuchukua fomu.

Watano katika kunyany’anyiro hicho alikuwa, Waziri wa Ujenzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Dk. Hussein Mwinyi ambaye ni mtoto wa Rais mstaafu wa Zanzibar na Tanzania, Ali Hassan Mwinyi.

Shamsi Vuai Nahodha, Waziri Kiongozi Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) alikuwa wa sita kuchukua fomu kasha akafuatia Mohammed Jaffar Jumanne, Mkurugenzi wa Ushindani wa Biashara Halali Zanzibar.

Wanane, alikuwa  Mohammed Hijja Mohammed na wa tisa akawa, Balozi Meja Jeneral mstaafu, Issa Suleimani Nassor.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!