Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwanajeshi aliyemsukuma Trafiki kwa gari kizimbani
Habari Mchanganyiko

Mwanajeshi aliyemsukuma Trafiki kwa gari kizimbani

Spread the love

 

ASKARI wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), MT 89487 CPL, Hamis Ramadhan, anayedaiwa kumsukuma askari wa usalama barabarani kwa kutumia gari lake, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam, kwa mashtaka ya kukataa amri halali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Ijumaa tarehe 24 Februari, 2023 na Jeshi la Polisi, Ramadhan amefikishwa mahakamani jana tarehe 23 Februari 2023 na kusomewa mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Rahim Mushi na Wakili wa Serikali, Vailer Kyendesya.

Akimsomea mashtaka hayo, Wakili Kyendesya amedai tarehe 7 Februari 2023, Ramadhan akiwa eneo la Mlimani City Barabara ya Survey, Kinondoni, jijini Dar es Salaam, akiendesha gari namba T. 433 ALB , aina ya Nissan Patrol alisimamishwa eneo la kivuko cha watembea kwa miguu na Askari Polisi, ambapo alikaidi na kuanza kumsukuma kwa gari yake.

Baada ya kusomewa shtaka hilo, Ramadhan alikana na kisha Wakili Kyendesya alidai upelelezi wa kesi hiyo umekamilika, hivyo anaiomba Mahakama kupanga tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.

Hakimu Mushi ameahirisha kesi hiyo hadi tarehe 6 Machi mwaka huu, kwa ajili ya kutajwa.

Hatua hiyo imekuja baada ya Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Jumanne Sagini kuliagiza Jeshi la Polisi kumkamata na kumchukulia hatua dereva huyo aliyeonekana kwenye video iliyosambaa mitandaoni akikaidi amri ya kusimama iliyotolewa na Askari wa usalama barabarani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!