Monday , 11 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Mwanaharakati achangia ujenzi ofisi serikali ya mtaa, barabara Dar
Habari Mchanganyiko

Mwanaharakati achangia ujenzi ofisi serikali ya mtaa, barabara Dar

Spread the love

MWANAHARAKATI huru, Bihimba Mpaya ameshirikiana na wadau wengine kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi wa Mtaa wa Magole A, uliopo Kivule, jijini Dar es Salaam, kwa kuchangia ujenzi wa ofisi ya Serikali ya mtaa na ukarabati wa barabara eneo la mlima Nyang’andu ambalo ni korofi wakati wa mvua. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Bihimba amekabidhi misaada hiyo katika nyakati tofauti kwa Mwenyekiti wa Mtaa wa Magole, Abubakari Kindagule.

Akizungumza baada ya kukabidhi misaada hiyo ikiwemo lori la mawe kwa ajili ya ukarabati wa barabara na nondo kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya serikali ya mtaa, Bihimba alisema amechukua uamuzi huo ili kuunga mkono jitihada za viongozi wa nchi kuwaletea maendeleo wananchi wake.

“Kwa muda mrefu wananchi wamekuwa wakipata shida ya barabara hususan wakati wa mvua, magari huwa yanakwama na hata kuhatarisha usalama wao kutokana na eneo la mlima Nyang’andu kuwa korofi. Serikali ya mtaa imejitahidi kutatua lakini nimeona bora niongeze nguvu kwa kutoa roli moja la mawe,” amesema Bihimba.

Kwa upande wake Kindagule, ameshukuru kwa msaada uliotolewa na Bihimba, akisema utasaidia kukamilisha ujenzi wa ofisi yake.

“Kwa muda mrefu mtaani kwetu tulikaa bila ofisi ya Serikali ya mtaa, tulikuwa tumepanga na changamoto za upangaji mnazijua. Kama mwenyekiuti nilinunua kiwanja hiki kwa ajili ya familia lakini nimelitoa kwa ajili ya ofisi kisha nikaanza kutafuta wadau kwa ajili ya kuniunga mkono,” alisema Kindagule na kuongeza:

“Namshukuru Bihimba amejitokeza kwa kutoa msaada wa ujenzi wa ofisi, lakini pia amechangia ukarabati wa eneo la barabara ambalo limekuwa kero kwa wananchi kwa muda mrefu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Amsons Group watoa milioni 100 waathirika maafa Hanang

Spread the loveKAMPUNI ya Amsons Group kupitia kampuni zake za Camel Oil...

Habari Mchanganyiko

Kesi ya mfanyakazi wa CRDB itaendelea J’tatu

Spread the love  MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kinondoni, Dar es Salaam inatarajia...

Habari Mchanganyiko

Mawasiliano Dar – Bagamoyo yarejea

Spread the loveMAWASILIANO ya barabara ya Mkoa wa Pwani na Dar es...

Habari Mchanganyiko

Tanesco: Mvua chanzo kukatika umeme leo

Spread the loveShirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limedai kuwa hitilafu iliyojitokeza katika...

error: Content is protected !!