Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Michezo Mwamyeto atua Yanga, Niyonzima Azam
Michezo

Mwamyeto atua Yanga, Niyonzima Azam

Spread the love

USAJILI wa wachezaji wa Ligi Kuu ya Vodamom Tanzania Bara kwa msimu ujao wa 2020/21 umeendelea kushika kasi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)

Mabingwa wa kihistoria, Timu ya Yanga imeendelea kuboresha ukuta wake kwa kumsajili beki kisiki wa Coastal Union ya Tanga na Timu ya Taifa ya Tanzania, Bakari Nondo Mwamnyeto.

Mwamnyeto amehitimisha uvumi wa wapi anakwenda msimu ujao kwa kusaini mkataba wa miaka miwili ya kutumia timu ya wananchi.

Upande mwingine, timu ya Azam FC ya Dar es Salaam nayo imekamilisha usajili wa kiungo mkabaji wa kimataifa wa Rwanda, Ally Niyonzima.

Niyonzima aliyekuwa akihusishwa kujiunga na Yanga, amesaini kandarasi ya miaka miwili kama mchezaji huru.

Kiungo hiyo alikuwa akikipiga Rayon Sports ya Rwanda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!