Tuesday , 5 December 2023
Home Kitengo Michezo Mwamuzi atupwa jela mwaka mmoja kwa kupanga matokeo
Michezo

Mwamuzi atupwa jela mwaka mmoja kwa kupanga matokeo

Spread the love

MAHAKAMA ya Mkoa wa Kilimanjaro, imemhukumu kifungo cha mwaka mmoja mwamuzi wa mpira wa miguu, Safiel Mjema baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kuomba na kupokea hongo ya Sh.120,000. Anaripoti Regina Mkonde, Kilimanjaro … (endelea).

Taarifa iliyotolewa jana Ijumaa tarehe 5 Juni 2020 na Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Mkoa wa Kilimanjaro, Fidelis Kalungura ilisema, hukumu hiyo ilitolewa tarehe 22 Mei 2020.

Alisema, hukumu hiyo ilikuwa ya kwenda jela mwaka mmoja au kulipa faini ya Sh. 500,000.

“Mtuhumiwa alishindwa kulipa faini hiyo hivyo alipelekwa jela kutumikia kifungo cha mwaka mmoja jela,” amesema Kalungura.

Alisema, mtuhumiwa huyo alifikishwa mahakamani hapo akikabiliwa na kosa la kuomba na kupokea hongo kiasi cha Sh.120,000 ili aweze kutoa upemndeleo kwa timu ya ‘New Generation’ iliyokuwa ikicheza na timu ya ‘La Familia’ kinyume cha kifungu cha 15 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na.11/2007.

“Tunatoa rai kwa wanamichezo kutojihusisha na vitendo vya rushwa kwa namna yoyote ile kwani vinadumaza maendeleo ya michezo na ustawi wa jamii yetu,” alisema Kalungura

“Vilevile, tunatoa rai kwa wananchi wote kuendeleza mapambano dhidi ya rushwa kwa kutoa taarifa kwa ofisi yetu iliyoko karibu au kupitia namba yetu ya dharura 113,” aliongeza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMichezo

Mwana FA anogesha Tamasha la Exim Bima Festival

Spread the loveNAIBU Waziri Wa Utamaduni, Sanaa Na Michezo, Hamis Mwinjuma ‘Mwana...

Michezo

Manchester City dhidi ya Tottenham ni usiku wa kisasi

Spread the love KIPUTE kati ya klabu ya Manchester City dhidi yaTottenham Hotspurs...

Michezo

Wikiendi ya kutamba na Meridianbet hii hapa usikubali kuikosa

Spread the loveMERIDIANBET wanakwenda kukupa nafasi ya kutambawikiendi hii kupitia ODDS KUBWA walizoweka...

Michezo

Fernandes hakamatiki Man Utd, mahesabu ni kuifunga Bayern

Spread the love  NAHODHA wa Manchester United, Bruno Fernandes, alikuwa na kiwango...

error: Content is protected !!