Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwakyembe awashukuru Watanzania
Habari Mchanganyiko

Mwakyembe awashukuru Watanzania

Spread the love

WAZIRI wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk.Harrison Mwakyembe, amewashukuru viongozi mbalimbali wa serikali na Watanzania wote kwa ujumla waliohusika kufanikisha shughuli nzima ya kumpumzisha mke wake Linah Mwakyembe, anaandika Irene David.

Ametoa shukrani hizo kwa niaba ya familia yake na kuongeza kuwa Watanzania wote wanastahili pongezi hizo.

Akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake Kunduchi Dar es Salaam leo, amesema kabla hajarejea ofisini kwake mjini Dodoma anawashukuru wananchi wote.

Shukrani hizo zimelenga Watanzania wote kwa ujumla wakiwepo wakazi wa Kyela alipozikwa mke wake, makanisa mbalimbali likiwemo kanisa la Moravian, Mashkeh akiwemo Mufti Mkuu na madaktari wote waliohusika kumsaidia marehemu.

Shukrani zingine alizitoa kwa wamiliki wa vyombo vya habari , watangazaji na waandishi wote wa habari waliofuatilia tangu ulipotokea msiba huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

error: Content is protected !!