Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwakibete: Watanzania someni vitabu kukuza maarifa
Habari Mchanganyiko

Mwakibete: Watanzania someni vitabu kukuza maarifa

Spread the love

NAIBU Waziri wa Wizara ya Miundo Mbinu na  Uchukuzi, Atupele Mwakibete ametoa wito kwa jamii  kuongeza juhudi katika kusoma vitabu ili kukuza maarifa.

Amesema usomaji wa vitabu unaisaidia jamii kupata  mbinu mbalimbali za uongozi  katika ngazi zote. Anaripoti Marry Victor…(endelea).

Mwakibete aliyasema hayo jana tarehe 15 Disemba, 2022 katika hafla ya uzinduzi wa kitabu kinachohusu masula ya Uongozi kiitwacho (Leadership through my lenses).

Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Habari na Teknolojia ya Mawasiliano Nape Nnauye; Mwakibete  alimpongeza mtunzi wa kitabu hicho Violet Mordechai na kuongeza kuwa  ili kupata viongozi wenye  maono na ubunifu ni muhimu kusoma vitabu.

“Uongozi unatafsirika kwa njia tofauti, siri kubwa ni kupata vitabu vyenye simulizi za kusisimua za uongozi na kuvisoma kisha kuyaishi yale uliyoyasoma yakuongoze kwenye shughuli zako,” amesema.

Mwakibete aliongeza kusema: “Nimekisoma ni kitabu kizuri naomba nakala za kitabu hiki zisambazwe kwenye ofisi na taasisi za umma ili nao wayaishi haya yaliyoandikwa humu.

“Hongera sana Violet kwa uandishi na ubunifu mkubwa ulioutumia katika kuandaa kitabu hiki,” alisema Naibu Waziri Mwakibete ambaye kwenye hafla huyo alimwakilisha Waziri wa Habari na Tehama, Nape Nnauye.

Naye mtunzi wa kitabu hicho Violeth aliwashukuru waliohudhuria katika hafla hiyo: uzinduzi huo huku akisisitiza ujumbe uliomo katika kitabu hicho kwamba uongozi ni kuonesha njia.

Katika uzinduzi huo muongoni mwa vitabu vilivyokabidhiwa kwa Naibu Waziri viliendelea kuuzwa ndani ya ukumbi huku akitoa ahadi ya kuvitumia vitabu hivyo wakati wowote pale itakapohitajika katika taasisi za serikali na umma kwa jumla.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!