Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwakabibi, wenzake wapandishwa kizimbani kwa uhujumu uchumi
Habari MchanganyikoTangulizi

Mwakabibi, wenzake wapandishwa kizimbani kwa uhujumu uchumi

Spread the love

 

ALIYEKUWA Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke, mkoani Dar es Salaam, Lusubilo Mwakabibi, amefunguliwa kesi ya uhujumu uchumi, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Leo Ijumaa, tarehe 20 Agosti 2021, Mwakabibi na mwenzake, Edward Haule, wamesomewa mashtaka mawili yaliyomo katika kesi hiyo na Wakili Serikali Mwandamizi, Ester Martin, mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi wa mahakama hiyo, Evodia Kyaruzi.

Wakili Martin aliyekuwa anasaidiana na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mkunde Mshanga, waliwasomea washtakiwa hao mashtaka ya matumizi mabaya ya madaraka na utumishi wa umma.

Mbele ya Hakimu Kyaruzi, Wakili Martin alidai kwamba, Mwakabibi na mwenzake walitenda kosa hilo kati ya Machi 2020 na Machi 2021, mkoani  Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa mashtaka hayo, Mwakabibi anadaiwa kutenda makosa hayo alipokuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke na Mratibu wa Mradi wa Uendelezaji Jiji la Dar es Salaam (DMDP).

Anadaiwa kutumia madaraka yake vibaya kwa makusudi, kwenda kinyume cha sheria ya ardhi.

Kufuatia uamuzi wake wa kuelekeza ujenzi wa stendi ya mabasi ya Buza, katika kiwanja ambacho ni mali ya Dayosisi ya Kanisa la Anglikana bila kupata ruhusa.

Baada ya washtakiwa hao kusomewa mashtaka, Hakimu Kyaruzi alitoa masharti ya dhamana ambayo, kila mshtakiwa alitakiwa kuwasilisha fedha taslimu Sh. 10 milioni, au mali isiyohamishika yenye thamani hiyo.

Pia kuwa na wadhamini wawili watakaosaini bondi ya Sh. 10 milioni.

Hata hivyo, Mwakabibi na mwenzake walishindwa kutimiza masharti ya dhamana hiyo.

Mahakama hiyo imewapa masharti washtakiwa hao, kuwasilisha mahakamani hapo hati ya kusafiria pamoja na  kutosafiri nje ya mkoa wa Dar es Salaam, bila kibali chake.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 2 Septemba mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!