Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mvua yaleta kizazaa Dar
Habari MchanganyikoTangulizi

Mvua yaleta kizazaa Dar

Spread the love

MVUA kubwa imenyesha jiji Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo Jumapili na bado inaendelea “kupiga” katika maeneo kadhaa jijini hapa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa kutoka maeneo mbalimbali za jiji hili zinasema, mvua nyingi imenyesha katika maeneo ya Kariakoo, Jangwani, Ilala, Kinondoni Bunju hadi Bagamoyo.

“Ukanda wote huu wa Pwani, mvua kubwa imenyesha na kwa mujibu wa taarifa ya hali hewa, mvua hizo zitaendelea kunyesha hadi Mei mwaka huu,” ameeleza mtaalam mmoja kutoka Idara ya hali hewa.

Mtaalam huyo ambaye hakupenda kutajwa jina kwa kuwa siyo msemaji wa Idara hiyo anasema, “utabiri unaonyesha kuna mvua kubwa zinazoweza kunyesha na huenda zikaleta maafa.”

Mwandishi wa habari hizi ameshuhudia magari kadha yakiwa yamekwama kwenye maji maeneo ya Kariakoo na Jangwani.

“Hapa Jangwani, kote kumejaa maji. Katika eneo la magari ya Mwendokasi, maji yamejaa na kuathiri kwa kiwango kikubwa usafiri,” ameeleza mmoja wa mashuhuda.

Katika eneo la Kariakoo, hasa barabara ya Nyerere aneo la Gerezani, magari kadhaa yalikwama na mengine kuzimika.

Kufuatia hali hiyo, baadhi ya vijana wanaofanya biashara ndogo ndogo katika maeneo hayo, walitumia fursa ya mkwamo; na au kuzimika wa magari hayo, kujipatia ajira.

Wengi wao walijitosa barabarani na kuanza kusaidia kukwamua baadhi ya magari yaliyokwama.

Kioja kikubwa kilikuwa pale gari la wagonjwa – Ambulance – lilizimika.

Baadhi ya vijana waliombwa kusaidia kulikwamua gari hilo, walilikwepa kwa hoja kuwa “mgonjwa hana hela.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!