Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mvua kubwa yatabiriwa Dar, Pwani
Habari Mchanganyiko

Mvua kubwa yatabiriwa Dar, Pwani

Mvua kubwa ikinyesha
Spread the love

MAMLAKA ya Hali ya Hewa nchini,( TMA) imetahadharisha ujio wa mvua kubwa kuanzia tarehe 23 Novemba 2018 hadi Aprili 2019, katika mikoa mbalimbali hasa Dar es Salaam na Pwani. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea). 

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 18 Oktoba 2018 na Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Agnes Kijazi wakati akitoa utabiri huo kwa wanahabari jijini Dar es Salaam.

Kijazi ameeleza kuwa, mikoa ya Dodoma, Singida, Tabora, Mbeya, Njombe, Iringa, Ruvuma, Kusini mwa mkoa wa Morogoro, Lindi na Mtwara inatarajiwa kupata mvua za wastani na za juu ya wastani, wakati mikoa ya Rukwa, Katavi, Kigoma na Songea ikitarajiwa kupata mvua za wastani hadi juu ya wastani.

Kufuatia utabiri huo, Kijazi amezitaka sekta mbalimbali zinazohusika na uchukuzi na mawasiliano, maji, nishati, mifugo na wanyamapori, usalama wa chakula na kilimo pamoja na afya, kuchukua tahadhari kufuatia mvua hizo ili kukwepa madhara yake.

“Mvua za msimu ni mahususi kwa maeneo ya magharibi mwa nchi, kanda ya kati, nyanda za juu kusini magharibi, kusini mwa nchi, ukanda wa pwani ya kusini pamoja na maeneo ya kusini mwa mkoa wa Morogoro ambayo yanayopata msimu mmoja wa mvua kwa mwaka,” amesema Kijazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!