Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Muuaji New Zealand kukumbwa na hukumu ya kihistoria
Kimataifa

Muuaji New Zealand kukumbwa na hukumu ya kihistoria

Spread the love

MTUHUMIWA wa mauaji ya watu 50 katika misikiti miwili iliyoko mjini Christchurch, New Zealand, Brenton Tarrant (28) huenda akakumbwa na adhabu ya kihistoria. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Terrant aliyeshtakiwa kwenye Mahakama ya Wilaya ya Christchurch kwa makosa 50 ya mauaji pamoja na makosa 39 ya kutaka kufanya majaribio ya mauaji katika misikiti hiyo, anatarajiwa kuwa mfungwa wa kwanza wa kifungo cha maisha jela pasipo kuwa na uwezekano wa kupewa msamaha kama ilivyo desturi ya taifa hilo.

Vyombo vya habari nchini humo vimeripoti kuwa, leo Alhamisi tarehe 4 Aprili 2019 ameongezewa mashtaka kadhaa, hali inayoashiria kwamba, mtuhumiwa huyo atakuwa wa kwanza kupewa adhabu ya kifungo cha maisha jela pasipo na uwezekano wa kupewa msamaha.

Kwa sasa Tarrant amewekwa rumande katika gereza lililoko mjini Auckland hadi pale kesi yake itakapopangiwa tarehe ya kutajwa na mahakama ya Christchurch, kwa ajili ya kusikilizwa.

Tarrant anadaiwa kufanya shambulizi la mauaji la risasi katika miskiti ya Al-Noor na Lin Wood wiki tatu zilizopita, na kusababisha vifo vya watu 50 na majeruhi 39.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!