Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mume wa Malikia Elizabeth afariki dunia
Kimataifa

Mume wa Malikia Elizabeth afariki dunia

Prince Pillip
Spread the love

 

MWANAMFALME Phillip (99), mume wa Malkia Elizabeth wa Uingereza, amefariki dunia asubuhi ya leo Ijumaa tarehe 9 Aprili 2021. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Kifo hicho kimetangazwa na Malkia Elizabeth ambapo taarifa yake imechapishwa katika ukurasa wa twitter wa Ikulu ya Buckingham, nchini humo.

Taarifa hiyo imeeleza “kwa masikitiko makubwa Mheshimiwa Malkia Elizabeth anatangaza kifo cha mume wake mpendwa, Mheshimiwa Mwanamfalme Phillip, mtawala wa Edinburg.”

Mtawala huyo wa Edinburgh, amefariki dunia asubuhi ya leo katika makazi ya kifalme yaliyopo Windsor Castor.

Mwanamfalme huyo alizaliwa katika Kisiwa cha Corfu tarehe 10 Juni 1921, ambapo baba yake alikuwa Mwanamfalme Andrew wa Ugiriki na Denmark. Mama wa mwanamfalme huyo alikuwa Mwanamfalme Alice.

Hayati Philip na Elizabeth walifunga ndoa mwaka 1947, ambapo miaka mitano baadaye Elizabeth alitawadhwa kuwa Malkia wa Uingereza.

Wawili hao wamejaaliwa kuwa na watoto wanne, wajukuu wanane na vitukuu 10. Kijana wao wa kwanza alikuwa Charles aliyezaliwa 1948, akifuatiwa na dada yake, Anne (1950), kisha Andrew (1960) na mwisho Edward (1964).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!