ABUBAKAR Zuberi, Mufti wa Tanzania kupitia Baraza Kuu la Waislam Tanzania (Bakwata), amelazwa kwenye Hospital ya Taifa ya Muhimbili kwa ugonjwa wambao haujatajwa. Anaandika Faki Sosi.
Taarifa kutoka ndani ya Bakwata zinaeleza kuwa, Mufti Zuberi alifikishwa Muhimbili jana baada ya kuugua ghafla.
Saidi Mpeta ambaye ni Ofisa Habari wa Bakwata amethibitisha kulazwa kwa Mufti Zuberi na kwamba alifikishwa Muhimbili jana.
Hata alipoulizwa ugonjwa unaomsumbua Mufti Zuberi, Mpeta hakutaka kuweka wazi ugonjwa huo na kudai taarifa itatolewa. Mufti Zuberi alichakuliwa kuwa Mufti wa Tanzania tarehe 10 Septemba mwaka jana.
More Stories
Bashungwa atoa maagizo 10 kwa waajiri na waajiriwa wapya
Gesi asilia kuinua uchumi wa wananchi
Watu 17 wafariki dunia kwa mkanyagano ‘Night Club’