Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Muarobani uuzwaji mafuta kwenye vidumu vijijini waja
Habari Mchanganyiko

Muarobani uuzwaji mafuta kwenye vidumu vijijini waja

Spread the love

NAIBU Waziri wa Nishati, Stephen Byabato amesema marekebisho ya kanuni za utengenezaji na uwekaji vituo vya mafuta katika maeneo ya vijijini, yanatarajiwa kukamilika Mei 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha…(endelea).

Byabato ametoa taarifa hiyo akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa wiki ya maji, iliyofanyika jijini Arusha, ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais, Dk. Phillip Mpango.

Amesema marekebisho hayo yatapelekea vituo vya uuzaji mafuta vijengwe kwa wingi maeneo ya vijijini, ambapo imependekezwa gharama zake zisizidi Sh. 7,000,000.

“Tunafanya mpango wa kurekebisha kanuni za utengenezaji na uwekaji vituo vya mafuta katika eneo la vijiji, ili kuhakikisha usalama wao ambao kwa sasa wanauza mafuta katika vidumu vya maji, waweze kupata vituo kwa gharama nafuu kwenye maeneo yao,” amesema Byabato na kuongeza:

“Kufikia Mei tutakuwa tumekamilisha kanuni na tungetamani na kupenda angalau kituo kinachowekwa katika maeneo ya vijijini kisigharimu zaidi ya Sh. 7 milioni ili huduma iwafikie wengi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

error: Content is protected !!