Thursday , 7 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Mtu mweusi apigwa risasi Marekani, maandamano yaibuka
Kimataifa

Mtu mweusi apigwa risasi Marekani, maandamano yaibuka

Spread the love

MAANDAMANO yameibuka jimbo la Wisconsin nchini Marekani baada ya polisi kutuhumiwa kumpiga risasi mtu mweusi nchini humo, Jacob Blake. Inaripoti BBC…(endelea)

Video zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii zimeonesha Blake akipigwa risasi kwa nyuma wakati anajaribu kuingia kwenye gari katika mji wa Kenosha.

Blake yupo hospitali akiendelea na matibabu huku mamlaka za Kenosha imetangaza hali ya dharura ya watu kutotoka nje baada ya kuzuka kwa maandamano.

Soma zaidi hapa

Mtu mweusi afanyiwa unyama Marekani

Mamia ya watu wameandamana hadi makao makuu ya polisi jana jumapili usiku na kuchoma moto magari huku waandamanaji wakipiga kelele wakisema hawawezi kurudi nyuma.

Tahadhari iliyotolewa kwa umma, polisi wamesema wanaofanya biashara saa 24 wafikirie kuzifunga kwasababu ya wizi na uvunjifu wa amani unaoweza kujitokeza.

Polisi wametumia mabomu ya machozi kutawanya mamia ya waandamanaji waliokiuka kauli ya kutotoka nje.
Gavana wa jimbo la Wisconsin, Tony Evers ameshutumu tukio hilo la kupigwa risasi Blake ambaye inasemekana hakuwa na silaha.

Evers amesema, wakati hana taarifa zote kwa sasa, anachojua ni kwamba huyo sio mtu wa kwanza kupigwa risasi au kujeruhiwa au kuuawa kiholela mikononi mwa polisi katika jimbo lao au nchi yao.

Idara ya haki ya Wisconsin inayochunguza tukio hilo, Imesema maafisa waliohusika wameagizwa kwenda likizo kwa uchunguzi zaidi.

Tukio hilo limetokea ikiwa imepitwa miezi michache tangu Afisa wa polisi mzungu kutuhumiwa kumuua raia wa Marekani, George Floyd.

Afisa huyo, Derek Chauvin aliyemkandamiza kwa mguu wake Floyd kisha kumfanya ashindwe kupumua na kupoteza maisha ameshtakiwa kwa mauaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

error: Content is protected !!