MUSSA Aboud Jumbe, amekuwa mwanachama wa 30 wa Chama cha Mapinduzi (CCM), kuchuchukua fomu ya kugombea Urais wa Zanzibar kupitia chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).
Jumbe ambaye ni Mtoto wa Rais wa awamu ya pili wa Zanzibar, Aboud Jumbe amekabidhiwa fomu hiyo leo Ijumaa tarehe 26 Juni 2020, katika Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui, na Cassian Gallo’s, Katibu wa Kamati Maalumu ya NEC Idara ya Oganaizesheni Zanzibar .
Akizungumza baada ya kukabidhiwa fomu hiyo, Jumbe amewataka Wazanzibar kumuombea ili afanikiwe katika mchakato huo.
“Nafahamu kabla yangu, wako wengi walishafika kwa ajili ya kupata ridhaa ya chama na baada ya hapo kupata ridhaa ya wananchi wa Zanzibar, nisingependa leo kuzungumza mengi sana, niwaombeni tu nanyi muwe pamoja nami,” amesema Jumbe
“Mniunge mkono katika kuniombea kwa Mungu lililokuwa lenye kheri liweze kufikia pale inapostahiki, baada ya hayo nisingelipenda kuzungumza zaidi,” amesema
Jumbe amekuwa mtoto wa tatu wa marais wastaafu kujitokeza kuchukua fomu ya kugombea urais wa Zanzibar, baada ya Dk. Hussein Mwinyi, Mtoto wa Rais Mstaafu wa Tanzania, Dk. Ali Hassan Mwinyi na Balozi Ali Abeid Karume, Mtoto wa Rais Mstaafu wa Zanzibar, Hayati Abeid Amana Karume.
Tangu zoezi la uchukuaji na urudishaji fomu, sambamba na utafutaji wadhamini lifunguliwe tarehe 15 Juni 2020, takribani watu 30 wamejitosa katika mchakato huo, ambapo wanawake waliojitokeza hadi sasa ni watatu na wanaume 27.
Wanawake waliojitokeza ni, Mwatum Mussa Sultan, Hasna Atai Masoud na Fatma Kombo Masoud.
Zoezi hilo linatarajiwa kufika tamati tarehe 30 Juni 2020, majira ya saa 10:00 jioni.
Wagombea wote 30 waliojitokeza ni;
- Mbwana Bakari Juma
- Balozi Ali Abeid Karume
- Mbwana Yahya Mwinyi :
- Omar Sheha Mussa
- Dk. Hussein Ali Mwinyi
- Shamsi Vuai Nahodha
- Mohammed Jaffar Jumanne
- Mohammed Hijja Mohammed
- Issa Suleiman Nassor
- Profesa Makame Mnyaa Mabarawa
- Mwatum Mussa Sultan
- Haji Rashid Pandu
- Abdulhalim Mohammed Ali
- Jecha Salum Jecha
- Dk. Khalid Salum Mohammed
- Rashid Ali Juma
- Khamis Mussa Omar
- Mmanga Mjengo Mjawiri
- Hamad Yussuf Masauni
- Mohammed Aboud Mohammed
- Bakari Rashid Bakari
- Hussein Ibrahim Makungu
- Ayoub Mohammed Mahmoud
- Hashim Salum Hashim
- Hasna Atai Masound
- Fatma Kombo Masound
- Iddi Hamadi Iddi
- Pereira Ame Silima
- Shaame Simai Mcha
- Mussa Aboud Jumbe
Leave a comment