Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mtoto wa Rais Jumbe ajitosa Urais Zanzibar, wagombea wafika 30
Habari za Siasa

Mtoto wa Rais Jumbe ajitosa Urais Zanzibar, wagombea wafika 30

Spread the love

MUSSA Aboud Jumbe, amekuwa mwanachama wa 30 wa Chama cha Mapinduzi (CCM), kuchuchukua fomu ya kugombea Urais wa Zanzibar kupitia chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

Jumbe ambaye ni Mtoto wa Rais wa awamu ya pili wa Zanzibar, Aboud Jumbe amekabidhiwa fomu hiyo leo Ijumaa tarehe 26 Juni 2020, katika Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui,  na Cassian Gallo’s, Katibu wa Kamati Maalumu ya NEC Idara ya Oganaizesheni Zanzibar .

Akizungumza baada ya kukabidhiwa fomu hiyo, Jumbe amewataka Wazanzibar kumuombea ili afanikiwe katika mchakato huo.

“Nafahamu kabla yangu, wako wengi walishafika kwa ajili ya kupata ridhaa ya chama na baada ya hapo kupata ridhaa ya wananchi wa Zanzibar, nisingependa leo kuzungumza mengi sana, niwaombeni tu nanyi muwe pamoja nami,” amesema Jumbe

“Mniunge mkono katika kuniombea kwa Mungu lililokuwa lenye kheri liweze kufikia pale inapostahiki, baada ya hayo nisingelipenda kuzungumza zaidi,” amesema

Jumbe amekuwa mtoto wa tatu wa marais wastaafu kujitokeza kuchukua fomu ya kugombea urais wa Zanzibar,  baada ya Dk. Hussein Mwinyi, Mtoto wa Rais Mstaafu wa Tanzania, Dk. Ali Hassan Mwinyi na Balozi Ali Abeid Karume, Mtoto wa Rais Mstaafu wa Zanzibar, Hayati Abeid Amana Karume.

Tangu zoezi la uchukuaji na urudishaji fomu, sambamba na utafutaji wadhamini lifunguliwe tarehe 15 Juni 2020, takribani watu 30 wamejitosa katika mchakato huo, ambapo wanawake waliojitokeza hadi sasa ni watatu na wanaume 27.

Wanawake waliojitokeza ni, Mwatum Mussa Sultan, Hasna Atai Masoud na Fatma Kombo Masoud.

Zoezi hilo linatarajiwa kufika tamati tarehe 30 Juni 2020, majira ya saa 10:00 jioni.

Wagombea wote 30 waliojitokeza ni;

  1. Mbwana Bakari Juma
  2. Balozi  Ali Abeid Karume
  3. Mbwana Yahya Mwinyi :
  4. Omar Sheha Mussa
  5. Dk. Hussein Ali Mwinyi
  6. Shamsi Vuai Nahodha
  7. Mohammed Jaffar Jumanne
  8. Mohammed Hijja Mohammed
  9. Issa Suleiman Nassor
  10. Profesa Makame Mnyaa Mabarawa
  11. Mwatum Mussa Sultan
  12. Haji Rashid Pandu
  13. Abdulhalim Mohammed Ali
  14. Jecha Salum Jecha
  15. Dk. Khalid Salum Mohammed
  16. Rashid Ali Juma
  17. Khamis Mussa Omar
  18. Mmanga Mjengo Mjawiri
  19. Hamad Yussuf Masauni
  20. Mohammed Aboud Mohammed
  21. Bakari  Rashid Bakari
  22. Hussein Ibrahim Makungu
  23. Ayoub Mohammed Mahmoud
  24. Hashim Salum Hashim
  25. Hasna Atai Masound
  26. Fatma Kombo Masound
  27. Iddi Hamadi Iddi
  28. Pereira Ame Silima
  29. Shaame Simai Mcha
  30. Mussa Aboud Jumbe

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!