Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mtoto wa Lowassa ajitosa ubunge Monduli
Habari za Siasa

Mtoto wa Lowassa ajitosa ubunge Monduli

Spread the love

FREDRICK, mtoto wa waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa, amechukua fomu ya kugombea ubunge Monduli, mkoani Arusha kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Fredrick amechukua fomu hiyo leo Jumanne tarehe 14 Julai 2020, katika Ofisi za CCM wilayani Monduli, mkoani Arusha na kukabidhiwa na Katibu wa chama hicho Wilaya ya Monduli, Langael Akyoo.

Mtoto huyo wa Lowassa amechukua fomu hiyo ili kujaribu bahati ya kuliongoza jimbo hilo, lililokuwa mikononi mwa baba yake tangu mwaka 1990 hadi 2015.

Lowassa aliliongoza jimbo hilo katika vipindi vitano mfululizo, kupitia Chama cha CCM.

Mwaka 2015 baada ya kuhamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), na kugombea urais na kuungwa mkono na vyama vya CUF, NLD na NCCR-Mageuzi vilivyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), jimbo hilo lilikwenda upinzani.

Julius Kalanga alishinda ubunge kupitia Chadema. Hata hivyo,  usiku wa tarehe 31 Julai 2018 alijiuzulu ubunge na kuhamia CCM ambako alipitishwa tena kuwania ubunge na kushinda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!