KAMPUNI ya ndege ya Precision imetoa taarifa ya uwepo wa mtoto mchanga mmoja miongoni mwa abiria 39 waliokuwa kwenye ndege iliyopata ajali Bukoba mkoani Kagera na kutumbukia Ziwa Victoria leo Jumapili tarehe 6 Novemba, 2022. Anaripoti Jonas Mushi, Dar es Salaam…(endelea)
Taarifa hiyo ambayo ni ya pili kwa umma iliyotolewa na kampuni hiyo imesema abiria wengine 38 ni watu wazima. Kampuni hiyo imesema watu 26 wameokolewa hadi sasa katika ajali hiyo lakini haijaweka wazi kama kichanga hicho ni miongoni mwao.
Taarifa hiyo ya Precision iliyowekwa kwenye mitandao wake ya kijamii, imesema hakuna vifo vilivyodhibitishwa hadi sasa na imetuma timu ya uchunguzi inayoundwa na maofisa wake na wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kuungana na timu ya uokozi. Kampuni hiyo itazungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam saa 9 kamili alasiri kuhusu ajali hiyo.
Ndege hiyo mruko namba PW 494 ilikuwa ikitokea jijini Dar es Salaam kuelekea Bukoba, imepata ajali na kutumbukia Ziwa Victoria asubuhi ya leo ikiwa na watu 43 miongonimwao abiria 39, wahudumu wawili na marubani wawili.
Taarifa ya awali iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera imeeleza zoezi la ukoaji linaendelea na kuna mawasiliano na marubani waliopo ndani ya ndege hiyo namba ATR-48 yenye usajili namba 5H-PWF.
Leave a comment