Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mtoto afariki kwenye ajali ya moto
Habari Mchanganyiko

Mtoto afariki kwenye ajali ya moto

Ulrich Matei Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya
Spread the love

MTOTO mmoja aliyefahamika kwa jina la Chriss Shida (2) amefariki dunia baada ya kuungua na moto akiwa nyumbani kwao katika kijiji cha Kimondo Wilayani Mbeya mjini. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 28 Agosti, 2018 SACP Ulrich Matei, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya amesema tukio hilo lilitokea jana majira ya saa mbili usiku.

Akielezea kuhusu tukio hilo, amesema chanzo cha moto huo ni mabanzi na majani ya jiko kuanguka wakati wahanga wako jikoni wanakula na kusababisha kushika moto na kuwaunguza.

Aidha, Kamanda Matei amesema mama mzazi wa marehemu aitwaye Maria Lucas alijeruhiwa na moto huo sehemu za mikononi na kifuani.

Kamanda Matei amesema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali teule ya Ifisi Mbalizi na mama wa marehemu anapatiwa matibabu hospitalini hapo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!