Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mtolea awahi kabla ya dirisha la usajili CCM kufungwa
Habari za SiasaTangulizi

Mtolea awahi kabla ya dirisha la usajili CCM kufungwa

Abdallah Mtolea, aliyekuwa Mbunge wa Temeke kwa tiketi ya CUF
Spread the love

YAMETIMIA. Mbunge wa Temeke, kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Abdallah Mtolea, hatimaye amejiuzulu nafasi hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Mtolea ametangaza kujiuzulu ubunge na uwanachama wa chama hicho kuanzia leo Alhamisi, tarehe 15 Novemba 2018.

Mbunge huyo amewahi kabla ya muda uliotangazwa na Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwa leo Novemba 15, 2018 ndiyo mwisho wa kupokea wabunge na madiwani kutoka katika vyama vya Upinzani na baada ya hapo hakuna atakayepewa nafasi ya kugombea tejna nafasi yake.

Mtolea leo ameutangazia umma kutokea bungeni jijini Dodoma kuwa amejiuzulu ubunge na nyadhifa zake zote kwenye chama chake, lakini hakuweka wazi anajiunga na chama gani.Mbunge huyo amesema sababu za kujivua ubunge na nafasi nyingine katika chama chake cha CUF mni kutokana na migogoro inayoendelea katika chama hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

error: Content is protected !!