Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mtobesya aahidi kuimarisha uhuru wa TLS , kuondoa ukata
Habari Mchanganyiko

Mtobesya aahidi kuimarisha uhuru wa TLS , kuondoa ukata

Mgombea Urais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), Jeremiah Mtobesya
Spread the love

 

MGOMBEA Urais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), Jeremiah Mtobesya, ameahidi kuimarisha uhuru wa chama hicho pamoja na kuongeza mapato yake, endapo atachaguliwa kushika wadhifa huo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mtobesya ametoa ahadi hizo leo Jumatano, tarehe 27 Aprili 2022, katika mdahalo wa wagombea urais wa TLS, uliofanyika jijini Dar es Salaam. Wagombea wengine ni, Profesa Edward Hoseah na Harold Sungusia.

“Suala lingine nitakalofanyia kazi ni independence of the bar (uhuru wa chama). Mawakili wenzetu mara nyingi tumewaona wakiingiliwa wakati wanafanya kazi zao, wakati mwingine anakuwa katika mgogoro na sheria bila sababu. Iwapo nitapata wasaa tutahakikisha tunawasaidia wakiwa kwenye mgogoro,” amesema Mtobesya.

Mtobesya amesema “tutatetea haki zao katika mfumo wa kistaarabu kwa kufuata sheria, sababu sheria zipo. Tutahakikisha haki ya wakili inapatikana bila kugandamiza haki yake.”

Aidha, ameahidi endapo atachaguliwa kuwa Rais wa TLS, atahakikisha chama hicho kinatekeleza majukumu yake katika kusimamia Bunge na Mahakama, kwa kutumia mpango kazi wake.

Mtobesya ameahidi endapo atachaguliwa, atasimamia maslahi ya mawakili wachanga.

“Ni ukweli usiopingika wadogo zetu wanapoingia sokoni wana struggle, si suala zuri kuwaacha waendelee ku-struggle, tumeshuhudia wengine wakikiuka maadili ili kuishi, nikichaguliwa tutafanya fund raising waji-organize kwenye vikundi kufungua kampuni kisha baadae watazirejesha ziwasaidie wengine,”a mesema Mtobesya.

Mtobesya ameahidi kufufua taasisi za TLS, ikiwemo Idara ya Maendeleo ya Biashara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!