Saturday , 3 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa
Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Sweetbert Nkuba
Spread the love

 

MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS), Sweetbert Nkuba amelaani kuenguliwa kwa jina lake kwenye hatua za awali za mchakato wa uchaguzi huo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, jana tarehe 23 Machi 2023, Nkuba alisema anatarajia kukata rufaa kupinga uamuzi huo uliotangazwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TLS, Charles Rwechungura hivi karibuni.

Nkuba alieleza kuwa anazo sifa za kuwa mgombea na kwamba ameshangazwa na kitendo cha kuenguliwa kwa jina lake kwa hoja ya kuwa aliwahi kuwa mtumishi wa serikali pia hakuwahi kuhudumu shughuli za uwakili kwa muda wa miaka kumi.

“Kwa mujibu wa sheria yetu na kanuni za uchaguzi za TLS nina sifa za kugombea …kulikuwa na hoja mbili hoja ya kwanza sikuwahi kufanya kazi ya uwakili kwa miaka kumi pili niliwahi kuwa mtumishi wa serikali sababu hizo sijakubaliana nazo kwani tangu nimeapishwa kuwa wakili huu ni mwaka wa 13 au 14 ni zaidi ya miaka 10 pili ni kweli nilikuwa mtumishi wa serikali na nilishaacha kazi serikalini kwa kufuata taratibu zote za kisheria kwa hiyo kamati imetumia maneno ya fununu kutoa uamuzi lakini sitaki kueleza sababu kiundani kwa kuwa nina jopo la mawakili walionipendekeza kuwania urais wakiongozwa na Jeremiah Mtobesya hivyo jopo linafanya utaratibu wa kukata rufaa,” alisema Nkuba.

Nkuba alisema kuwa anataka kukata rufaa ili haki ionekane imetendeka lakini pia kuhakikisha uwepo wa demokrasia kwenye vyama vyote vya kitaaluma ili kitendo hicho kisijitokeze tena.

Dk. Aloyce Rugazia Wakili wa Nkuba ambaye atamwakilisha mbele ya kamati ya Rufaa ya TLS alisema kuwa kigezo kilichotumika kumng’oa mteja wake ni cha kibaguzi kwakua kufanya kazi serikalini haiwezi ikamtia Wakili dosari kiasi hicho.

“Mteja wangu alinipigia simu nikapitia uamuzi uliotolewa na kamati na nimeona kuwa kuna mambo yanahitaji ufafanuzi kwa sababu yanaibua utata kwa mfano wanasema mteja wangu alikuwa mtumishi wa serikali kwa hiyo kwa mujibu wa taarifa za TLS mteja wangu amefanya kazi ya uwakili miaka miwili wanajaribu kutoa kile kipindi alichotumikia serikali mimi naona ni ubaguzi kwa watu waliotumikia serikali,” alisema Rugazia.

Dk. Rugazia alisema kuwa watafika mbele ya kamati ya Rufaa ya TLS ili kupata tafsiri ya kufanya kazi ya uwakili kwa kipindi cha miaka kumi kuna hesabiwa kwa kigezo kipi.

“Nafikiri tafsiri ya kufanya kazi ya uwakili iangaliwe ni lini alitunikiwa cheti cha uawakili ni ni lini alikabidhiwa cheti cha uwakili nafikiri ni uamuzi unaotakiwa utazamwe upya” alisema Dk. Rugazia.

Dk Rugazia alisema kuwa rufaa yao ikigonga mwamba mbele ya kamati basi watalazimika kutoka nje kwenda Mahakama Kuu kukata rufaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Magunia 731 ya bangi yakamatwa, mamia ya hekari yateketezwa Arumeru

Spread the love  MAMIA ya magunia ya madawa ya kulevya aina ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yakabidhi eneo la mahakama ya Afrika ya haki za binadamu

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa...

Habari Mchanganyiko

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni

Spread the loveBENKI ya NMB imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Asasi...

error: Content is protected !!