Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mtendaji Ruaha asimulia njama za kutaka kumuua zilivyopangwa
Habari MchanganyikoTangulizi

Mtendaji Ruaha asimulia njama za kutaka kumuua zilivyopangwa

Spread the love

MTENDAJI wa tarafa ya Ruaha, wilayani Ulanga, mkoani Morogoro, George Kayora, ameieleza mahakama jinsi baadhi ya viongozi  wa  ngazi ya kitongoji wilayani Ulanga, walivyoshirikiana na wananchi kula njama za kutaka kumuua. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea)

Kayora alieleza hayo juzi wakati akitoa ushahidi wake kwenye kesi ya shambulio la kuhudhuru mwili lililotokea Juni 17 2022, katika kitongoji cha Kitope, wilayani Ulanga, mkoani  Morogoro.

Kayora ambaye ndiye shahidi wa kwanza katika kesi hiyo, alidai mbele ya Mahakama ya wilaya ya Ulanga kwamba waliohusika kula njama za kutaka kumuua  ni  baadhi ya viongozi wa ngazi ya kitongoji.

Akiongozwa na Mwendesha Mashitka wa Jamhuri, Inspekta Rajabu, Kayora aliwataja viongozi aliodai wamekula njama kutaka kumuua kuwa ni Osward, (Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kitope, kijiji cha Mzelezi) na Charles Madonda (Katibu wa CCM, kata ya Chirombola).

Aliendelea kudai kuwa viongozi hao ambao wote  ni washitakiwa katika kesi hiyo, walishirikiana na mchimba madini aliyemtaja kwa jina la Dendelege, kufanya shambulio hilo ambalo nusura auawe.

Aliendelea kueleza kuwa viongozi hao waliwakusanya wananchi na kutoa maagizo ya kumshambulia mtendaji huyo wakati akitekeleza majukumu yake.

Alidai alikwenda katika eneo la kijiji cha Kitope kusimamia utekelezaji wa agizo la Mkuu wa Wilaya ya Ulanga, Ngolo Malenya aliyeagiza kutoruhusu shughuli za uchimbaji madini unaofanywa kiholela katika eneo hilo ambalo ni hifadhi ya barabara.

“Mheshimiwa hakimu, viongozi hawa ndio waliokula njama kwa kushirikiana na wananchi ili wanishambulie kwa lengo la kutaka kuniua, alidai Kayora.

Alieleza kuwa siku ya tukio wakati akienda kwenye eneo la machimbo ya madini ya rubi, kwa namna ya kustaajabisha Osward alimsimamisha barabarani akiwa na kundi la wananchi, kisha Madonda aliwaamuru wananchi kumshambulia.

“Wakati wananchi wananishambulia, viongozi hao waliungana na wananchi, wakaendelea kutoa maelekezo ya kuhamasisha wanipige.

“Nilipigwa kwa mawe, magongo na kukatwa na kitu chenye ncha kali mkono wangu wa kushoto na kusababisha kuvuja damu nyingi sana,” alidai Kayora

Pia alidai katika shambulio hilo, aliteguka bega lake la kulia na kupata maumivu makali yaliyopelekea apate rufaa katika Hospital ya Mtakatifu Francis ya Ifakara, akitokea hospitali wilaya ya Ulanga, mkoani Morogoro.

Alieleza mahakama kuwa ana mshukuru mkuu wa wilaya ya Ulanga, Ngolo Malenya  na viongozi wote wa wilaya chini ya Mkurugenzi Mtendaji kwani walipambana kuokoa maisha yake na kufanikiwa kuwanasa wahusika ambao wapo hapo mahakamani.

Tukio la kushambuliwa kwa mtendaji huyo, pia lililaaniwa vikali na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala  za Mikoa na Serikali Za Mitaa (TAMISEMI), Innocent Bashungwa na kuagiza wahusika wafikishwe kwenye mikono ya sharia.

Kesi hiyo itaendelea kusikilizwa tena Agosti 18 mwaka huu mahakamani hapo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

error: Content is protected !!