Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Mtanzania afungwa miaka 110 kwa ugaidi Kenya
Habari Mchanganyiko

Mtanzania afungwa miaka 110 kwa ugaidi Kenya

Nyundo ya Hakimu
Spread the love

RAIA wa Tanzania, Abdul Harun Karim amefungwa miaka 110 jela nchini Kenya,  kwa makosa ya kujihusisha na vitendo vya kigaidi nchini humo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).  

Karim alihukumuiwa kifungo hicho na Mahakama ya Lamu mbele Hakimu Mkuu wa mahakama hiyo, T.A. Sitati tarehe 22 Mei 2019, baada ya kukutwa na hatia katika mashitaka sita ya ugaidi yaliyokuwa yana mkabili nchini humo.

Miongoni mwa mashitaka yaliyo kuwa yana mkabili Karim ni pamoja, na kuwa gaidi wa kigeni, kuhamia nchini Somalia kwa lengo la kufundishwa masuala ya ugaidi na ukusanyaji wa taarifa kinyume na sheria ya kuzuia masuala ya ugaidi nchini Kenya.

Katika hukumu hiyo, ushahidi umethibitisha kwamba Karim alikutwa katika Kisiwa cha Kiwayu kilichopo Lamu  akiwa anajirekodi video iliyobeba ujumbe wa ‘bomu la kujitoa muhanga’ miaka mitatu iliyopita.

Aidha, katika shitaka lake lililokuwa lina mkabili la kuwa raia wa kigeni mwenye kujihusisha na masuala ya ugaidi Kenya, Karim alifungwa miaka 30 jela baada ya kukutwa na hatia.

Kwa mujibu wa mashitaka yaliyomtia hatiani Karim, mfungwa huyo alikamatwa mnamo tarehe 9 Mei 2019 kwenye kisiwa cha Kiwayu akiwa njiani kuelekea nchini Somalia kwa ajili ya kufundishwa masuala ya ugaidi. Ambapo mahakama hiyo ilimhukumu miaka 20 jela kwa kosa hilo.

Hakimu Sitati aliamuru Karimu kutumikia miaka 30 na 20 jela kwa wakati mmoja, kisha kutumikia kifungo cha miaka 60 jela kama adhabu ya makosa manne yaliyokuwa yana mkabili, ambapo kifungo hicho ni sawa na miaka 15 jela kwa kila kosa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi wa wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu

Spread the love  KAMISHNA wa Polisi Utawala Menejimenti ya rasilimali watu, CP...

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

error: Content is protected !!