Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mtanzania afungwa miaka 110 kwa ugaidi Kenya
Habari Mchanganyiko

Mtanzania afungwa miaka 110 kwa ugaidi Kenya

Nyundo ya Hakimu
Spread the love

RAIA wa Tanzania, Abdul Harun Karim amefungwa miaka 110 jela nchini Kenya,  kwa makosa ya kujihusisha na vitendo vya kigaidi nchini humo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).  

Karim alihukumuiwa kifungo hicho na Mahakama ya Lamu mbele Hakimu Mkuu wa mahakama hiyo, T.A. Sitati tarehe 22 Mei 2019, baada ya kukutwa na hatia katika mashitaka sita ya ugaidi yaliyokuwa yana mkabili nchini humo.

Miongoni mwa mashitaka yaliyo kuwa yana mkabili Karim ni pamoja, na kuwa gaidi wa kigeni, kuhamia nchini Somalia kwa lengo la kufundishwa masuala ya ugaidi na ukusanyaji wa taarifa kinyume na sheria ya kuzuia masuala ya ugaidi nchini Kenya.

Katika hukumu hiyo, ushahidi umethibitisha kwamba Karim alikutwa katika Kisiwa cha Kiwayu kilichopo Lamu  akiwa anajirekodi video iliyobeba ujumbe wa ‘bomu la kujitoa muhanga’ miaka mitatu iliyopita.

Aidha, katika shitaka lake lililokuwa lina mkabili la kuwa raia wa kigeni mwenye kujihusisha na masuala ya ugaidi Kenya, Karim alifungwa miaka 30 jela baada ya kukutwa na hatia.

Kwa mujibu wa mashitaka yaliyomtia hatiani Karim, mfungwa huyo alikamatwa mnamo tarehe 9 Mei 2019 kwenye kisiwa cha Kiwayu akiwa njiani kuelekea nchini Somalia kwa ajili ya kufundishwa masuala ya ugaidi. Ambapo mahakama hiyo ilimhukumu miaka 20 jela kwa kosa hilo.

Hakimu Sitati aliamuru Karimu kutumikia miaka 30 na 20 jela kwa wakati mmoja, kisha kutumikia kifungo cha miaka 60 jela kama adhabu ya makosa manne yaliyokuwa yana mkabili, ambapo kifungo hicho ni sawa na miaka 15 jela kwa kila kosa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!