Tuesday , 21 March 2023
Home Kitengo Michezo Mtangazaji mpira azua kioja uwanjani
Michezo

Mtangazaji mpira azua kioja uwanjani

Spread the love

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida Mtangazaji wa mpira nchini Urusi ameondoka uwanjani kabla mchezo haujaisha na kuwaacha watazamaji wakiangalia mechi hiyo bila maelezo.

Wakati wa mechi hiyo kati ya klabu ya Urusi ya Torpedo Vladmir dhidi ya Tekstilshchik Ivanovo kipa wa Ivanovo alimuangusha mshambuliaji wa upinzani kulingana na kanda za video.

Wakati wa tukio hilo timu hizo mbili zilikuwa 1-1. na baada ya kutolewa mkwaju wa penalti refa alitoa mkwaju wa adhabu nje ya eneo hatari na kusababisha malalamiko kutoka kwa mashabiki na watazamaji.

Na wakati mkwaju huo wa adhabu ulipopigwa mmoja ya walinzi waliunawa mpira na kuzua madai ya mkwaju mwingine wa penalti lakini refa aliwaambia wachezaji kuendelea na mchezo hatua iliyomlazimu mtangazaji huyo kumshutumu vikali refa huyo.

Hatua hiyo ilimkasirisha mtangazaji huyo na kuamua kusitisha matangazo aliyokuwa akitoa kulingana na ripoti za Pravda.

Na baada ya shutuma hizo ambapo mtangazaji huyo alimtajwa kwa jina la Nikolsky. “Aibu kubwa kwa soka ya Urusi, aliinuka na kuondoka huku akisema tazameni mechi bila mtangazaji leo.”

Mechi hiyo ilikamilika kwa timu zote mbili kufungana kwa bao 1-1.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!