Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mtangazaji ITV auwawa
Habari Mchanganyiko

Mtangazaji ITV auwawa

Marehemu, Blandina Sembu, Mtangazaji wa kipindi cha Jarida la Wanawake
Spread the love

 

BLANDINA Sembu, Mtangazaji wa kipindi cha Jarida la Wanawake kinachorushwa na kituo cha runinga cha ITV, ameuawa na watu wasiojulikana. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumapili tarehe 28 Machi 2021, na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni, Ramadhan Kingai.

Kamanda Kingai amesema kuwa, mwili wa marehemu Sembu ulitupwa maeneo ya njia panda ya ITV, mbele ya Baa ya MaryLand, na watu wasiojulikana, waliokuwa wakitumia gari aina ya Toyota Noah.

Kamanda Kingai amesema baada ya mwili huo kuchunguzwa, ulikutwa na majeraha maeneo ya usoni.

Amesema Jeshi la Polisi mkoani humo lilipata taarifa kutoka kwa raia wema jana Jumamosi tarehe 27 Machi 2021, majira ya saa tano usiku.

“Tulichobaini katika uchunguzi wa awali marehemu hakuuliwa pale, mauwaji yalifanyika sehemu nyingine. Amekutwa na majeraha sehemu za usoni ambapo inaonekana alipigwa na kitu kizito usoni wakati anapambana kujitetea,” amesema Kamanda Kingai.

Kamanda Kingai amesema uchunguzi juu ya mauwaji hayo unaendelea kufanywa na Jeshi la Polisi Kinondoni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!