Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Msuya: Mjadala wa Katiba uishe
Habari za SiasaTangulizi

Msuya: Mjadala wa Katiba uishe

Spread the love

WAZIRI Mkuu mstaafu, Cleopa Msuya amesema ingependeza iwapo mchakato wa Katiba mpya ungefikia mwisho, ili kuruhusu Watanzania kufanya kazi, huku akisisitiza elimu ya urai kwa wananchi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea)

Msuya aliyasema hayo leo tarehe 19 Julai, 2022 baada ya kuwasilisha maoni yake mbele ya Kikosi Kazi cha Rais Samia Suluhu Hassan cha kuratibu  maoni ya wadau wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa.

Ushauri wa Mzee Msuya kuhusu Katiba mpya ni mwendelezo wa viongozi waandamizi ambao wamepata nafasi ya kutoa maoni mbele ya Kikosi Kazi cha Rais Samia akiwemo Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), mstaafu Jaji Damian Lubuva, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mstaafu Profesa Mussa Assad.

Pia hitaji la Katiba mpya limezungumziwa na Katibu Mkuu Kiongozi mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, Jukwaa la Katiba Tanzania (JUKATA) na wengine.

Waziri Mkuu huyo mstaafu amesema ni vizuri suala la  Katiba kufikia mwisho,  huku akishauri iwapo kuna taarifa mpya za kuongezwa mchakato ufanyike ili Katiba ipatikane.

Amesema haipendezi kila mwaka Watanzania kurudia kudai Katiba kila mara na kwamba watu wanatakiwa kufanya kazi kujenga nchi yao.

“Serikali ifikirie namna ya kufunga mjadala wa kupatikana Katiba mpya, ili watu walijenge Taifa lao badala ya kuendelea kusikia mijadala ya  Katiba kiloa kukicha,” amesema.

Kuhusu ni kitu gani kitambulie kati ya Tume Huru ya uchaguzi na Katiba Mpya, Waziri Mkuu Msuya alisema suala la kujua sehemu ya kuanzia waachiwe viongozi wa Serikali, huku akisisitiza kuwa mjadala wa Katiba unatakiwa kufikia mwisho.

Msuya amesema Rais Samia ameanza kazi vizuri, hivyo ni jukumula la kila Mtanzania kumuunga mkono ili kuchochea mafanikio ambayo yameanza kuonekana.

“Haya mambo ya kupanga kipi kitangulie waachiwe viongozi wetu wa kiserikali ndio wanaojua mambo zaidi lakini nataka mjadala wa Katiba mpya umalizike upesi iwezekanavyo kwa uratibu ambao watajipanga wao,” amesema Msuya.

1 Comment

  • Jamani samahani Sana mmeniacha nyuma Sana. Kwanza naomba kujua Tume ya Mh. Jaji Waryoba MAONI ya Nchi yalifikia wapi? Na Serkali umeshindwa Nini kukamilisha au KUTOA MSIMAMO. Kama Tena tumeunda Kikosi KAZI Cha kuratibu MAONI mapya, kweli hii sio doublication ya MAONI ya katika. Hamuoni kuwa mnatuchanganya. Pia hamuoni kuwa hii NI gharama juu ya gharama?
    Sisi KAZI yetu kubwa NI Kueachagua viongozi watuwakilishe katika maamuzi Bora na sahihi.
    Tunaomba wawakilishi wetu katika vikao vyao halali wahalalishe MAONI ya wananchi. Hatuwezi kuongozwa kwa kujaza MAONI tuu, Bali maamuzi ni ya wale tuliowaamini kutuwakilisha.
    MAONI yatachukuliwa hata miaka kumi, majibu NI yaleyale tu. Hivyo fanyieni KAZI hayo Kwanza. Katiba sio biblia au Jirani. Hivyo hitaji likiibuliwa kwa wakati huo, tutalishughulikia kwa muda huo. Hayo tuliokusanya yangu enzi za Jaji Waryoba Hadi Kikosi KAZI, yanatosheleza kwa mahitaji yetu ya leo.
    Mungu ibariki Tanzania na Viongozi wake wote.
    AMEN.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!