Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Msukuma: Nagu umetumwa?
Habari za Siasa

Msukuma: Nagu umetumwa?

Spread the love

PENDEKEZO la wabunge kutaka kuwabebesha mzigo wananchi kwa kuongeza Sh. 50 kwa kila lita ya mafuta ya petroli na dizeli, limesababisha wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kushutumiana. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).    

Pendekezo hilo linalenga kutanua mfuko wa maji limewaingiza kwenye ‘vita’ Dk. Mary Nagu, Mbunge wa Hanang (CCM) ambaye anapendekeza mzigo huo atwishwe mwananchi huku Joseph Kisheku (Musukuma), Mbunge wa Geita (CCM) akipinga.

Dk. Nagu akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Maji kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 tarehe 3 Mei 2019, aliwataka wabunge kukubali azimio la kuongeza kiasi hicho cha fedha ambazo zitatoka kwa wananchi wanunuapo dizeli na petroli.

Maelezo ya Dk. Nagu yalimtibua Msukuma ambapo aliomba taarifa kwa Job Ndugai, Spika wa Bunge, hata hivyo hakuruhusiwa.

Baada ya kuona haruhusiwi, Msukuma alisimama na kusema “mama nakuheshimu sana aisee!” kauli hiyo ilimfanya Dk. Nagu kumsikiliza na kumpa nafasi Msukuma aendelee.

Ndipo Musukuma alipomtaka Dk. Nagu alithibitishie Bunge kama ametumwa na wafanyabiashara wa petroli, na kama hakutumwa, basi afute kauli yake.

Pamoja kauli ya Msukuma, Dk. Nagu aliendelea kusimamia msimamo wake kwamba, mzigo huo uelekezwe kwa wananchi huku akimtaka Msukuma kuvumiliana.

“Musukuma asikubali wenye petroli wamtumie huku ndani kuwa hiyo pesa (Sh. 50) isitokane na petroli,” amesema Dk. Nagu.

Katika maelezo yake ya awali, Dk. Nagu alisema, mfuko wa maji umefanikisha miradi mingi na kwamba, kuimarika kwa mfuko huo kutachochea miradi mingine.

Amesisitiza kwamba, kama Bunge litarudi nyuma, juhudi za maji zitarudi nyuma huku akitaka vyanzo vingine vitafute kwa ajili ya miradi ya maji.

Kurushiana maneno kwa wabunge hao kulitokana na Musukuma kutaka wabunge kutokubali kuongeza kiasi hicho cha fedha katika mafuta kwani kufanya hivyo ni kuwabebesha wananchi mzigo.

Amesema kuondokana na tatizo la maji matatizo katika sekta nyingine pia yataondoka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!