Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Msomi IFM adakwa akitaka kukodisha Bastola
Habari Mchanganyiko

Msomi IFM adakwa akitaka kukodisha Bastola

Spread the love

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam imemtia mbaroni mwanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Robson Maji (21)kwa kosa la kukutwa akitaka kuuza bunduki aina ya Bastola yenye risasi, anaandika Faki Sosi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo ofisini kwake Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema kuwa mwanafunzi huyo alikamatwa akiwa kwenye mipango ya kuuza Bastola aina ya Beretta yenye namba DAA316502 ikiwa na risasi sita.

Mambosasa amesema kuwa jeshi hilo lilipata taarifa ya kuwepo kwa biashara ya kukodishwa kwa silaha kwa majambazi ili wakafanyie kazi za kiuhalifu na kulipwa fedha na kwamba uliandaliwa mtego maeneo ya TRA Mwenge na kumkamata mtuhumiwa akitaka kukodisha kwa Sh.. 400,000.

Mtuhumiwa huyo aligunduliwa kuwa yupo tayari kuiuza kwa Sh. 2,500,000 na kwamba alipohojiwa alikiri kuiba silaha hiyo kwa Baba yake aitwaye Isaack Maji (51) mkazi wa Tabata Segerea.

Mtuhumiwa baada ya kuhojiwa alitaja mshirika wake ambaye ni rafiki yake mwanafunzi wa Chuo cha Columbus Staste Cummunity cha nchini Marekani.

Amesema upelelezi unaendelea ili kujua mmiliki halali wa silaha hiyo na mahojiano zaidi yanafanyika ili kuweza kubaini silaha hiyo imekodishwa mara ngapi na imetumika na watu gani

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!