Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Msiba wa Ruge wakwamisha kesi ya Halima Mdee
Habari za SiasaTangulizi

Msiba wa Ruge wakwamisha kesi ya Halima Mdee

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeahirisha usikilizaji wa kesi ya uchochezi inayomkabili Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, kufuatia shahidi wa upande wa mashitaka kushindwa kufika mahakamani. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Wakili wa Serikali, Ashura Mzava ameiambia mahakama kuwa shahidi huyo ameshindwa kufika mahakamani kutoa ushahidi wake, kutokana na msiba wa bosi wake, Ruge Mutahaba. 

Shahidi aliyeshindwa kufika Mahakamani, ni Abdul Mchembea, mfanyakazi wa Clouds Media Group Limited (CMG). Amefiwa na bosi wake – mkurugenzi wa matangazo -aliyefariki dunia juzi tarehe 26 Februari 2019, nchini Afrika Kusini.

Taarifa zinasema, Ruge alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya ini na figo.

Kesi hiyo ambayo iko mbele ya Thomas Simba, Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, ilikuja kwa ajili ya kusikilizwa.

Hakimu Simba amesema, kutokana na dharura hiyo kesi imeahirishwa mapaka tarehe 21 Machi mwaka huu.

Mdee anadaiwa kutenda kosa hilo tarehe 3 Julai 2017 akiwa makao makuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mtaa wa Ufipa, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa hati ya mashitaka, Mdee anatuhumiwa kutamka maneno kuwa “anaongea hovyo hovyo, anatakiwa afunge breki;” na kwamba kitendo hicho kingeweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!