Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Michezo Mshambuliaji wa Burundi afunga usajili Yanga
Michezo

Mshambuliaji wa Burundi afunga usajili Yanga

Fiston Abdul Razak
Spread the love

KUELEKEA kufungwa kwa dirisha dogo la usajili, klabu ya Yanga imefanikiwa kumsajili mshambuliaji wa kimataifa kutoka Burundi, Fiston Abdul Razak ili kuongeza nguvu kwenye eneo la ushambuliaji. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mshambuliaji huyo mwenye miaka 27, huenda akawa anafunga usajili ndani ya klabu hiyo kwenye dirisha dogo mara baada ya kufanikiwa kuwanasa Saidi Ntibazonkiza pamoja na Dikson Job kutoka Mtibwa.

Kupitia mitandao ya kijamii ya klabu hiyo ilimtambulisha Fiston kama mchezaji wao mpya mara baada ya kitendawili cha muda mrefu.

Uongozi wa klabu hiyo umeamua kufanya usajili wa mshambuliaji mara baada ya kutolizishwa na viwango vya washambuliaji waliopo kwa sasa licha ya timu hiyo kuongoza Ligi mpaka sasa na kutopoteza mchezo wowote.

Fiston ambaye ni mchezaji tegemeo kwenye timu ya Taifa ya Burundi ameshawahi kucheza kwenye klabu za Mamelodi Sundown ya Afrika Kusini na Sofapaka ya Kenya katika maisha yake ya mpira.

Kwa usajili huo huenda akaenda kuongeza nguvu kwenye eneo la ushambuliaji ambapo mara nyingi alikuwa akicheza Michael Sarpong ambaye ameonekana kutokuwa na makali.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Ujanja ni kubeti na Meridianbet

Spread the love  JUMAPILI ya leo imekaa kihela hela sana ndani ya...

Michezo

Anza Jumamosi yako na mkwanja wa Meridianbet

Spread the loveJumamosi ya leo ODDS zimekaa kijanja sana ndani ya Meridianbet...

error: Content is protected !!