Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Msemaji wa White House ya Trump aachia ngazi
Kimataifa

Msemaji wa White House ya Trump aachia ngazi

Sean Spicer, Msemaji wa Rais wa Marekani
Spread the love

MSEMAJI wa rais wa Marekani, Donald Trump amejiuzulu kufuatia uteuzi wa rais wa mkurugenzi mpya wa mawasiliano nchini humo, anaandika Catherine Kayombo.

Sean Spicer, amejiuzulu kwa kutofurahishwa na mabadiliko hayo ya uongozi katika idara ya mawasiliano, akidai kuwa kuwepo kwa mkurugenzi wa mawasiliano katika Ikulu ya White house kutaleta utata katika utendaji kazi wake.

Spicer hajaridhishwa na uteuzi wa Anthony Scaramucci, mfadhili wa kampuni ya Wall Street kuwa mkurugenzi wa idara ya mawasiliano.

Amefananisha mabadiliko hayo na uwepo wa wapishi wengi jikoni na kwamba kunaweza sababisha kuharibu mapishi.

Msemaji huyo wa zamani amekuwa akimtetea rais Trump na kuvishutumu vyombo vya habari kuwapotosha Wamarekani kuhusu uongozi wa Trump.

Vikao vyake na wanahabari vimekuwa maafuru na mara nyingi huzuia mijadala ya mawazo kati ya wanahabari hasa wale wasiokubaliana na uongozi wa Trump.

Aidha, Trump amemshukuru Spicer kwa kazi aliyoifanya hasa kumtetea mbele ya wanahabari nchini humo.

Amekuwa akimtetea rais hata katika madai ya Urusi kuingilia uchaguzi wa Marekani mwaka uliyopita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!