Saturday , 10 June 2023
Home Kitengo Maisha Afya MSD yawatangazia ‘neema’ wagonjwa
Afya

MSD yawatangazia ‘neema’ wagonjwa

Spread the love

BOHARI ya Dawa hapa nchini (MSD) leo imetangaza hali ya kuridhisha ya upatikanaji wa dawa na kusema hadi kufikia mwishoni mwa mwezi huu aina 17 ya dawa zitawasili kwamba upatikanaji wa dawa unategemewa kuwa asilimia 86, anaandika Pendo Omary.

Laurean Rugambwa, Mkurugenzi Mkuu – MSD leo amewaambia waandishi wa habari kwamba, “hadi kufikia Februari mwaka huu aiana tatu za dawa zitawasili na hali ya upatikanaji wa dawa inategemewa kuwa asilimia 88.” 

“Vilevile hadi kufikia mwezi Machi 2017 tunatarajia aina mbili za dawa zitawasili na hali ya upatikanaji wa dawa inategemewa kufikia asilimia 90 na hivyo kuwepo kwa aina 100 za dawa kati ya 135 ya dawa zote muhimu,” amesema Rugambwa.

Rugambwa amesema kwa upande wa dawa za miradi Msonge ambazo zinatibu na kuzuia magojwa ya Malaria, UKIMWI, Kifua Kikuu, Ukoma, Kichaa cha Mbwa, uzazi wa mpango na chanjo mbalimbali dawa hizo zipo kwa asilimia 100.

Itakumbukwa kuwa, mwishoni mwa mwaka jana taarifa iliyotolewa na taasisi isiyo ya kiserikali inayofuatiiia masuala ya Afya inayojulikana kwa jina la Sikika ilisema kuwa MSD inakabiliwa na upungufu wa dawa na kueleza kuwa kuna makopo 173 tu ya dawa aina ya Paracetamol nchini.

Taarifa hiyo iliungwa mkono na baadhi ya wananchi wakiwemo waonjwa katika wilaya mbalimbali hapa nchini walioeleza kuwa upatikanaji wa dawa na chanjo kwa watoto ulikuwa mgumu. Taarifa ambazo zilikuwa zikikanushwa vikali na Wizara ya Afya.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Afya

GGML yaadhimisha siku ya mazingira duniani kwa kutoa elimu kuhusu taka za plastiki

Spread the loveKAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited (GGML) ambayo ni moja...

Afya

TEMDO yaanza kuzalisha vifaa tiba, bilioni tatu kutumika

Spread the loveKATIKA kukabiliana na changamoto ya upatikanaji wa vifaa tiba nchini,...

Afya

Ummy Mwalimu:Umeme wa uhakika tija kwa uboreshaji huduma za afya

Spread the loveWAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu amepongeza juhudi zinazoendelea kufanywa na...

Afya

Madaktari bingwa 10 waliokuwa India warudi na shuhuda nzito kuhusu utalii tiba

Spread the loveMADAKTARI bingwa wa upasuaji wa ubongo wameendelea kuongezeka katika Taasisi...

error: Content is protected !!