RAPA maarufu nchini Afrika Kusini, Kiernan Forbes ‘AKA’ ameuawa akiwa amesimama nje ya mgahawa mmoja huko Durban jana usiku.
Kwa mujibu wa taarifa za vyombo vya habari nchini humo, inadaiwa kuwa magari mawili yalipita na kufyatua risasi muda wa saa 10 jioni kwa saa za huko. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa …(endelea).
Rapa huyo alitakiwa kutumbuiza katika klabu ya usiku iitwayo YUGO usiku huo wa Ijumaa.
Taarifa ilichapishwa kwenye mitandao ya kijamii, ikisema kuwa hafla hiyo ilighairiwa kutokana na hali zisizotarajiwa.
Inadaiwa kuwa AKA alipigwa risasi sita, huku mwanaume mwingine naye akidaiwa pia kuuawa kwenye tukio hilo.
Rapa mzaliwa wa Cape Town, aliingia kwenye tasnia hiyo baada ya kuachia wimbo wa Victory Lap kutoka kwenye albamu yake ya kwanza, Altar Ego mwa 2011.
Albamu hiyo ilishinda tuzo kadhaa na mwaka 2021 alitangazwa kuwa msanii bora wa kiume wa mwaka katika tuzo za muziki za Afrika Kusini.
Aliendelea kufanikiwa na albamu yake ya pili Levels mwaka 2014, ikifuatiwa na yake ya tatu, Touch My Blood, mwaka 2018.
AKA alichumbiana kwa muda mfupi na DJ Zinhle na mwaka 2015 walifanikiwa kumpata binti Kairo.
Aidha, msanii huyo alishirikiana na wasanii wa Tanzania Joh Makini katika wimbo wa Donbother huku Staa Diamond Platnumz akishirikiana naye katika wimbo wa Make me sing.
Leave a comment