MVUTANO kati ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Tanzania na Chama cha NCCR-Mageuzi umeanza upya, hivyo ndivyo unaweza kusema. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam …(endelea).
Hivi karibuni ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ilitangaza kuandaa kikao kitakachoshirikisha wadau wa siasa ili kupata ufumbuzi wa malalamiko ambayo yalitolewa na vyama vya siasa, kikiwemo NCCR-Mageuzi kuwa Jeshi la Polisi linavunja Sheria ya Vyama vya Siasa.
Baada ya kutangaza kikao hicho, vyama vya NCCR-Mageuzi, Chadema na ACT-Wazalendo vilitangaza kutoshiriki, hali ambayo inatajwa kusababisha kikao hicho kuahirishwa.
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa 21 Oktoba 2021, iliandika barua yenye Kumb. Na. HA. 322/362/18/11, ikitaka chama hicho kuwasilisha maelezo ambapo Mkuu wa Idara ya Uenezi na Mahusiano ya Umma wa chama hicho, Edward Simbeye alisema wanaona barua hiyo inauhusiano na msimamo wao.
Barua ya Msajili wa Vyama vya Siasa ambayo imeandikwa na Naibu Msajili, Sisty Nyahoza, ilisema wamepokea malalamiko kutoka kwa mwanachama wa chama hicho, Yeremia Maganja akieleza kuwa, uchaguzi wa Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu Tanzania Bara na Wajumbe wa Kamati Kuu wa chama hicho uliofanyika 16 Januari 2021, haukufuata utaratibu ulioelezwa katika Katiba na Kanuni za chama chao, hivyo ni batili.
Undani wa habari hii, kujua barua husika na majibu ya NCCR- Mageuzi kwenda kwa msajilim soma Gazeti la Raia Mwema, toleo la leo Jumatatu tarehe 8 Novemba 2021.
Leave a comment