Wednesday , 27 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Msaidizi wa Zitto ‘aokotwa’ Kenya
Habari Mchanganyiko

Msaidizi wa Zitto ‘aokotwa’ Kenya

Spread the love

RAPHAEL Ongangi, aliyekuwa Msaidizi wa Zitto Kabwe, Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo amepatikana akiwa hai asubuhi ya leo tarehe 2 Julai 2019, eneo la Mtwapa mjini Mombasa, Kenya. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Taarifa za kupatikana kwa Ongangi zimetolewa leo mchana na mke wake, Veronica Kundya akisema kwamba, mumewe amepatikana akiwa salama mjini Mombasa.

Veronica amesema, amewasiliana na mumewe kwa njia ya simu na kumhakikishia kwamba, yuko salama.

Veronica amemshukuru Mungu pamoja na watu wote waliojitokeza kupaza sauti zao, tangu Ongangi alipotekwa na watu wasiojulikana tarehe 24 Juni 2019 jijini Dar es Salaam.

“Nipo hapa leo nikiwa na furaha kubwa sana sana kuushuhudia ukuu wa Mungu. My Raphael (Ongangi) amepatikana leo Mombasa na yupo salama, sina taarifa zingine zaidi ya hiyo, ila hiyo pia inatosha sana kwangu. 

“Napenda kuwashukuru wote kwa moyo wangu wote kwa niaba ya familia yangu kwa sala na kujitoa kwenu kwa hali na mali kwenye kipindi hiki kigumu. Mimi na familia yangu tutaishi kutangaza ukuu wa Mungu

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari Mchanganyiko

Wizara ya madini kurusha ndege ya utafiti wa madini Geita

Spread the loveKutokana na mchango wa wachimbaji wadogo wa madini kwenye pato...

Habari Mchanganyiko

Jafo aagiza kampuni za madini kuzingatia utunzaji mazingira, azitaka zijifunze kwa GGML

Spread the loveWAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia apewa tano ujenzi barabara Mtwara

Spread the loveWANANCHI wa Mkoa wa Mtwara, wameishukuru Serikali ya Rais Dk....

error: Content is protected !!