Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Msaidizi wa Sabaya aibua utata kesi ya Mbowe
Habari za SiasaTangulizi

Msaidizi wa Sabaya aibua utata kesi ya Mbowe

Freeman Mbowe akiwasili mahakamani Kisutu
Spread the love

 

SHAHIDI wa pili wa Jamhuri, Justine Elia Kaaya leo Alhamisi tarehe 28 Oktoba 2021, ameendelea kutoa shahidi katika kesi inayomkabili kiongozi wa chama kikuu cha upinzani Tanzania cha Chadema, Freeman Mbowe na wenzake. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Ni katika Mahakama Kuu, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Dar es Salaam mbele ya Jaji Joackim Tiganga.

Kaaya aliyekuwa msaidizi wa Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya, ameibua utata baada ya kudai alikutana na Mbowe, kipindi ambacho mwanansiasa huyo anadaiwa kuwa katika mahabusu ya Gereza la Segerea.

Baada ya jana Jumatano tarehe 27 Oktoba 2021, wakati akiongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Abdallah Chavula, kutoa ushahidi wake, mahakamani hapo mbele ya Jaji Joachim Tiganga, kudai alikutana na Mbowe Januari 2020.

Lakini leo Alhamisi, Wakili Kibatala alimhoji Kaaya alikutana na Mbowe tarehe ngapi na yeye alikamatwa tarehe ngapi, ambapo amejibu akidai, alikamatwa tarege 25 Agosti 2020 na alikutana na Mbowe Oktoba 2020.

Aidha, akiulizwa na Wakili Chavula leo, ufafanuzi wake kuhusu tofauti ya tarehe alizokutana na Mbowe, amejibu akidai suala hilo lilitokea sababu wakili wa utetezi alimuuliza katika wakati sio sahihi hivyo alimchanganya na kwamba wakati sahihi aliokutana na Mbowe ni Oktoba 2018 na sio Oktoba 2020.

Jana akitoa ushahidi wake, Kaaya alidai kwamba Mbowe aliwahi kumfuata na gari lake lenye usajili wa KUB, ambalo ni la Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, mwanzoni mwanzoni mwa 2020.

Wakili Kibatala alimhoji kama anafahamu kuwa Mbowe alinyang’anywa hadharani gari hilo, ambaye amejibu akidai hafahamu.

Fuatilia mahojiano hayo kati ya Wakili wa utetezi, Peter Kibatala na Kaaya.

Kibatala: Kwa Ruhusa yako Mheshimiwa Jaji naomba kuuliza maswali yakibakia nitaomba Michael Mwangasa amalizie.

Kibatala: Shahidi unakumbuka jana wakati wa ushahidi wako ulitaja namba zako za Simu

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Unaweza kunitajia

Shahidi: 0693006700 na 0754916666

Kibatala: Unajua umekuja kutoa ushahidi kwenye kesi nzito?

Shahidi: Shahidi sijui kesi nzito, najua nimekuja kutoa ushahidi tuh

Kibatala: Unakumbuka wakati unaandika maelezo yako kwa Inspector Swila ulitoa namba zako za simu

Shahidi: Hapana sikutoa

Kibatala: Kwa Ruhusa ya mahakama unaweza kusoma hapa

Shahidi: 0754 216170

Kibatala: Je unasemaje kuhusu hizo namba?

Shahidi: Sijui sasa

Kibatala: Je iambie Mahakama chini ya kiapo hizi namba sasa Inspector Swila kazitoa wapi

Shahidi: Sijui

Kibatala: Shahidi unaweza kutuambia aliyethibitisha maelezo ya Inspector Swila kuwa maelezo ni sahihi ni nani

Shahidi: Ni mimi

Kibatala: Shahidi tuambie wakati unatoa namba za simu hapa Mahakamani umetoa ushahidi au kielelezo kama usajili kwamba ni namba za kwako

Shahidi: Hapana

Kibatala: Unamfahamu Inspector Swila kwa kumuona

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Ni mmoja ya aliyekuwa anawalinda mahakamani wakati wa kesi

Shahidi: Hapana

Kibatala: Jana wakati unatoa ushahidi ulisema ujawahi kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa

Shahidi: Ndiyo, sijawahi

Kibatala: Ujawahi kushiriki kura za maoni kata ya Pili?. Kama nikileta ushahidi ulishiriki

Shahidi: Walete mahakamani

Kibatala: Tutarudi hapo baadae

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Nimesikia umesema kuwa umeishi na Sabaya na ukasema ulikuwa unaishi naye akiwa na mke wake. Je ulitutajia jina la mke wa Sabaya

Shahidi: Nilitaja jina Moja la Jesca

Kibatala: Je uliishi na Sabaya kwa muda gani akiwa mkuu wa wilaya

Shahidi: Miezi mitatu

Kibatala: Unafahamu mahala anapoishi mkuu wa wilaya ni mahala nyeti

Shahidi: Sahihi

Kibatala: Unafahamu makazi ya mkuu wa wilaya ni Ikuku ndogo ya hilo eneo

Shahidi: Sahihi

Kibatala: Unafahamu kuwa kuna baadhi ya vikao vya kiusalama vinafanyika kwa mkuu wa wilaya

Shahidi: Sahihi

Kibatala: Je wewe ulifanyiwa vetting na tasisi yoyote?

Shahidi: Hapana

Kibatala: Na ulikuwa na access ya kuachiwa nyumba na ukaingia popote kwa mkuu wa wilaya

Shahidi: Sahihi

Kibatala: Nimeona pia una jina lingine la Power Kaaya, umelitoa wapi

Shahidi: Tangu nikiwa nyumbani

Kibatala: Nitakuwa sahihi nikisema umepewa hilo jina baada ya kufanya uhalifu sana maeneo ya Longido na Arusha?

Shahidi: Hapana si kweli

Kibatala: Nitarudi eneo hilo baadae

Kibatala: Je unafahamu wakati unakutana na Freeman Mbowe ulikuwa unafahamu ni mwalifu

Shahidi: Sijui

Kibatala: Wakati unakutana na Mbowe ulikuwa unajiskia amani kukutana naye pekeyako?

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Wakati unampa majina ulitambua kuwa yanakwenda kutendewa uhalifu

Shahidi: Ndiyo nilijua kuwa kuna halufu ya uhalifu

Kibatala: Una elimu gani

Shahidi: Kidato cha nne

Kibatala: Kwa hiyo uliona uhalifu wa madawa ya kulevya unatolea taarifa wapi

Shahidi: Polisi

Kibatala: Je wakati Mbowe anakupatia pesa Sh.200,000 ulijua ilikuwa kwa ajili ya uhalifu?

Shahidi: Hapana alisema ilikuwa ni ya usumbufu

Kibatala: We uliamini kuwa ni ya usumbufu?

Shahidi: Ndiyo

Kibatala Mwambie Mheshimiwa Jaji Je uliriport polisi?

Shahidi: Ndio

Kibatala: Ulisema baada ya kukutana na Mbowe ulimpigia simu Mbunge na Sabaya

Shahidi: Hapana

Kibatala: Je kazi ya Mbunge ni kushughulika na uhalifu

Shahidi: Ndiyo wao ni watunga Sheria

Kibatala: Je ulimwambia Mheshimiwa Jaji baada ya kutoa taarifa kwa Mbunge ulifuatilia kama amefanyia kazi taarifa hiyo

Shahidi: Hapana sikufuatilia

Kibatala: Shika maelezo yako haya kielelezo D1 uliyoyatoa kwa Inspector Swila kama ulimwambia mambo ya kihalifu aliyokwambia Mbowe

Shahidi: Haipo

Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa taarifa yako ya jana ya Sh.200,000 ulitolea maelezo kwa Inspector Swila

Shahidi: Haipo

Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji kuwa ulimpigia Sabaya simu, Je ulitaja namba za simu za Sabaya

Shahidi: Sikuzitaja

Kibatala: Ulimwambia Jaji kuwa baada ya kumkosa Sabaya ulifanya jitihada za kumtafuta Sabaya

Shahidi: Sikumwambia

Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji kuwa baada ya kumkosa Sabaya ulimtafuta mke wa Sabaya huyo Jesca kwamba kuna taarifa mbaya ya Sabaya

Shahidi: Sikusema

Kibatala: Uliowataja jana ni walinzi wa Sabaya

Shahidi: Hapana ni marafiki zake

Kibatala: Hao uliokuwa umewataja jana ulikuwa umefahamiana nao kwa muda mrefu au mfupi

Shahidi: Muda mfupi

Kibatala: Je uliwataarifu hao marafiki wa Sabaya

Shahidi: Hapana

Kibatala: Wakati unakutana na Freeman Mbowe ulihisi uhalifu gani unataka kufanyika

Shahidi: Sikuwa nafahamu

Kibatala: Mkutano wa kwanza unaosema mlikutana na Mbowe, kama kweli ilikuwa lini

Shahidi: 2020 mwezi wa kumi, sikumbuki tarehe

Kibatala: Nilisikia kuwa umesema walikufuata na gari, Je gari ya KUB?

Shahidi: Ilikuwa gari ya kiraia

Kibatala: Unasema alikuwa anaendesha mwanamke?

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Angalia maelezo yako hapo, Je umeeleza kuhusu huyo mwanamke. Je, ulifahamu kuwa Mbowe alikuwa anakwambia mambo ya kihalifu ila ukaenda kuonana naye

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kuna mahala yoyote ulitoa taarifa kama polisi hivi ndiyo ukaenda kukutana naye

Shahidi: Sikutoa

Kibatala: Ulipokamatwa 20-08 -2020 ulihifadhiwa Gereza gani?

Shahidi: Ukonga

Kibatala: Lakini ulikutana na Mbowe Longido Oktoba 2020

Kibatala: Okeeeey kazi yangu kuuliza maswali. Haya mara ya pili mlikutana na Mbowe wapi na lini

Shahidi: Mwanzoni mwaka 2020

Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji ni wapi katika Statement ataona Khalfani Bwire alikwepo Katika Kikao Moshi

Shahidi: Khalfani Bwire alikuwa katika kikao cha tatu

Kibatala: Sawa mwambie sasa katika hayo maelezo yako ni wapi ulimwambia Inspector Swila kuwa Khalfani Bwire alikwepo?

Shahidi: Hakuna

Kibatala: Nini kilitangulia kati ya maelezo yako na ushahidi wako mahakamani

Shahidi: Kilitangulia maelezo

Kibatala: Je wewe ulitambua Bwire wapi?

Shahidi: Kabla ya mahakamani

Kibatala: Kwa hiyo kumtambua Bwire umefanya jana hapa mahakamani

Shahidi: Nilimwambia kabla

Kibatala: Kwa hapo kwenye maelezo ipo sehemu umemtaja Bwire?

Shahidi: Hapana

Kibatala: Kwa hiyo sisi tunaona umefanya hivyo kwa mara ya kwanza jana

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Mliongea nini

Shahidi: Wao ndiyo walikuwa wananielezea walivyokuwa wanamtafuta Sabaya

Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Mambo mazito kama hayo katika Statement hiyo atayaona ukurasa wa ngapi

Shahidi: Hayapo

Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kuwa mambo mazito kama hayo ulisema kuwa uliripoti mambo mazito kama hayo kwa Mkuu wa Gereza

Shahidi: Sikusema

Kibatala: Inawezekana wewe na Inspector Swila mlipitiwa sasa mwambie Mheshimiwa Jaji kama uliriport Matukio kama hayo popote

Shahidi: Sikusema

Kibatala: Je ulizungumzia ulikamatiwa wakati unapelekea pesa benki

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Ukasema ulikuwa na Dollar na Euro

Shahidi: Sahihi

Kibatala: Ukasema ulikuwa unafanya biashara na Hotel gani

Shahidi: Mount Meru

Kibatala: Je ulitoa kielelezo chochote kama ulilipwa fedha hizo

Shahidi: Sikutoa

Kibatala: Ulifafanua kwa Mheshimiwa Jaji kwamba ulibadili pesa kwa Euro na Dollar kwenda fedha za Kitanzania

Shahidi: Nilifafanua jana kuwa nilipewa pesa ambalimbali

Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kuwa ulitoa nyaraka za malipo za Mount Meru

Shahidi: Sikutoa

Kibatala: Ulitaja jina la afisa aliyekulipa hizo pesa

Shahidi: Sikutoa

Kibatala: Mount Meru hawanunui papo kwa papo wanafanya kazi kwa mkataba na mzabuni. Je, ulitoa Mkataba kwa Jaji

Kibatala: Ulitoa risiti za TRA na zingine kwamba biashara ni halali

Shahidi: Sikutoa

Kibatala: Je unataka Mount Meru Hotel Leo wasikie wanapo fuatilia kesi hii wasikie luxury walikulipa Dollar 1000 cash

Shahidi: Siyo Mount Meru bali mtu wa mount Meru

Kibatala: ooohooo uliiyasema hayo jana

Shahidi: Sikusema

Kibatala: Polisi walipokukamata unawakumbuka.?

Shahidi: Siwakumbuki

Kibatala: Unasema ulihojiwa na Inspector Mahita

Shahidi: Ndiyo kuhusu tuhuma zote

Kibatala: Mahojiano uliyafanyia wapi

Shahidi: Central Dar es Salaam

Kibatala: Mashitaka yalifutwa na Ukakabidhiwa fedha zako

Shahidi: Ndiyo nilirudishiwa

Kibatala: Walichukua hivi hivi au walikuandikisha na kukupa karatasi

Shahidi: Walinipa karatasi

Kibatala: Je wakati jana mawakili wa serikali waliokuongoza walikuonesha hapa mahakamani hiyo karatasi

Shahidi: Hapana hawakunionyesha

Kibatala: Swala la pesa ni kubwa sana, je ulionesha karatasi kwamba sasa wamenirudishia

Shahidi: Sikuonesha

Kibatala: Unaweza kutuambia huyo Wakili wa Serikali ambaye badala ya  kukwambia uende kwa DPP badala yake akakawambia uende Central

Shahidi: Sikumbuki

Kibatala: Sisi tunasema kuwa hizo Euro au Dollar hujarudishiwa

Shahidi: Wamenirudishia.

Kibatala: Haya niambie sasa kuhusu kukutana na Freeman Mbowe Je ulitoa taarifa hapa mahakamani kuwa mlinzi wake sikuwa namfahamu vizuri

Shahidi: Hapana

Kibatala: Je ulimwambia Mheshimiwa Jaji baada ya kuombwa majina mara ya pili ulichukua tahadhari za kwenda polisi

Shahidi: Sikusema

Kibatala: Je ulimwambia Sabaya mwenye rafiki zake kuwa kuna jambo linaendelea wachukue tahadhari

Shahidi: Sikusema

Kibatala: Zile fedha ulizopokea ulizionaje za kiharifu au fedha safi

Shahidi: Niliona fedha safi

Kibatala: Baada ya kuona siyo pesa mbaya ndiyo maana hukumwambia Sabaya, mke wa Sabaya, wala marafiki zake

Shahidi: Hapana si kweli

Kibatala: Je mwambie sasa Mheshimiwa Jaji hayo majina yamo katika Statement?

Shahidi: Hayamo

Kibatala: Namba zao za simu?

Shahidi: Hazimo

Kibatala: Hilo gari la KUB uliona lini

Shahidi: Januari 2020

Kibatala: Unataka Mahakama ikuchukulie wewe ni shahidi muhimu na umetoka kwa mchumba wako kuja kutoa ushahidi

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Je, unafahamu Januari 2020, Freeman Mbowe alikuwa gerezani Segerea baada ya kufutiwa dhamana Mahakama ya Kisutu

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Je mtu akiwa gerezani Segerea anaweza kukutana na wewe Longido

Shahidi: Hapana sifahamu

Kibatala: Umezungumzia Joyce Mukya jana, nieleze kwenye statement hiyo umeandika wapi

Shahidi: Hakuna mahala nilipoandika

Kibatala: Kwetu muhimu sana sijui Kwa Mahakama

Kibatala: Je kuna karatasi umetoa hapa Mahakamani inayoinesha ushahidi wa kwamba namba hii ilimpigia namba hii, Je ulitoa karatasi hiyo hapa Mahakamani

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!