Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Msafara wa Kigwangalla wapata ajali, mmoja afariki
Habari MchanganyikoTangulizi

Msafara wa Kigwangalla wapata ajali, mmoja afariki

Spread the love

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla amepata ajali alfajiri ya leo tarehe 4 Agosti, 2018 kwenye eneo la Magugu mkoani Manyara akiwa safarini akitokeaArusha kuelekea Dodoma. Anaripoti Regina Kelvin…(endelea).

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Augustino Senga amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambapo amesema Afisa wa Habari wa Wizara hiyo, Hamza Temba aliyekuwa kwenye msafara wa waziri amefariki dunia.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, RPC Ramadhan Ng’azi Rpc amethibitisha taarifa za ajali hiyo ambapo amesema Waziri Kigwangalla amepata ajali hiyo Mkoani Manyara alipokuwa njiani akitokea Arusha kuelekea Dodoma.

“Ajali alipata mkoani Manyara, alikuwa Arusha kikazi akaondoka alfajiri kuelekea safari yake nafikiri Dodoma alipofika Manyara tukapewa taarifa kwamba amepata ajali,” amesema RPC Ng’azi.

Taarifa zinasema Dk. Kigangwalla anaendelea vizuri na anapelekwa hospitali ya Mount meru Arusha pamoja na msaidizi wake ambaye ameumia sana kwa kutumia helkopta kutoka Magugu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tanzania yakabidhi rasmi msaada nchini Malawi

Spread the loveWAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,...

Habari Mchanganyiko

Bashe: Tumeshagawa pikipiki 5,500 kati ya 7,000 kwa maafisa ugani

Spread the love  WAZIRI wa Kilimo, Hussen Bashe, amesema wizara hiyo tayari...

Habari Mchanganyiko

Spika Tulia awapa neno mawaziri utekelezaji mashamba ya pamoja

Spread the love  SPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, amewataka mawaziri kushirikiana...

Habari Mchanganyiko

Ukosefu wa maadili kwa wakunga, wauguzi bado changamoto

Spread the loveIMEELEZWA kuwa vitendo vya uvunjifu wa maadili kwa  wauguzi na...

error: Content is protected !!