Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mrithi wa Ndugai: CCM yasogeza vikao mbele
Habari za SiasaTangulizi

Mrithi wa Ndugai: CCM yasogeza vikao mbele

Rais Samia Suluhu Hassan, Mwenyekiti wa CCM
Spread the love

 

CHAMA tawala nchini Tanzania- Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimesogeza mbele vikao vyake kikiwamo cha kamati kuu kutoka jana Jumanne, tarehe 18 Januari 2022 hadi kesho Alhamisi, jijini Dodoma. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Ratiba ya awali ya vikao hivyo vyenye lengo la kuchakata na kumpata mrithi wa Job Ndugai, aliyejiuzulu nafasi ya spika wa Bunge la Tanzania, tarehe 6 Januari 2022, ilikuwa vinafanyika kwa siku mbili yaani jana na leo Jumatano.

Jumla ya wagombea 70 wamejitosa kuwania nafasi hiyo ya uongozi wa muhimili wa Bunge.

Leo Jumatano, tarehe 19 Januari 2022, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Shaka Hamud Shaka ametoa taarifa kwa umma kikao cha kamati kuu kitafanyika tarehe 20 Januari, 2022 badala ya tarehe 18 Januari, 2022 katika ofisi za Makao Makuu (White House), Dodoma.

           Soma zaidi:-

“Kikao hicho kitatanguliwa na kikao cha sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa. Maandalizi ya vikao vyote hivyo yamekamilika,” amesema Shaka

Kikao hicho cha kamati kuu, kitakuwa na jukumu zito la kuwafyeka wagombea 67 kati ya 70 waliojitosa kwenye kinyanyany’iro hicho na kubaki na majina matatu ambayo yatapelekwa katika kamati ya wabunge wa CCM.

Kamati ya wabunge wa CCM, itakuwa na jukumu la kumchagua mmoja ambaye atakwenda kukiwakilisha chama kwenye uchaguzi wa spika utakaofanyika tarehe 1 Februari 2022, siku ya kwanza ya mkutano wa kwanza wa Bunge la sita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!