Thursday , 18 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mrisho Gambo ‘awapiga mkwara’ wafugaji
Habari Mchanganyiko

Mrisho Gambo ‘awapiga mkwara’ wafugaji

Makundi ya Ng'ombe yaliyokutwa katika Poro Tengefu la Loliondo
Spread the love

MKUU wa Mkoa Arusha, Mrisho Gambo amesema mwananchi yeyote atakayeshindwa kutoa ushirikiano wa kujua idadi ya mifugo aliyo nayo atatiwa nguvuni, anaandika Mwandishi Wetu.

Akizungumza wakati wa kuzindua kazi ya ukusanya takwimu iliyofanyika kwenye kata ya Olbalbald, alisema serikali imeamua kufanya sensa ili kujua idadi sahihi itakayoweza kuwasaidia wananchi wa eneo hilo kupata misaada.

“Kujua idadi ya mifugo itatusaidia serikali kujua hata kama tunaleta chanjo za mifugo basi tujue ni idadi gani na pia kujua mifugo iliyo ni ya eneo hilo au la,” alisema.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Baraza la Wafugaji, Edward Maura, alisema kupitia ukusanyaji wa takwimu ya idadi ya watu na mifugo kwenye eneo hilo, litaweza kusaidia kutoa dira ya maendeleo hasa katika kubainisha maeneo pamoja na matumizi yake.

Amesema eneo hilo linakabiliwa na changamoto nyingi ikiwamo uhaba wa maji, barabara na huduma za kijamii kwa hiyo amesema kujua idadi halisi ya watu itawezesha kutengeneza fursa za kimaisha na kimaendeleo ya wananchi pamoja na serikali.

Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Takwimu, Jocye Saul, alisema ukusanyaji wa sensa umekuwa shirikishi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

Habari Mchanganyiko

Serikali yatoa ajira watumishi 46,000, yatangaza utaratibu mpya kuajiri

Spread the loveSERIKALI imetangaza nafasi za ajira za watumishi wa umma 46,000...

error: Content is protected !!