Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Mrisho Gambo ‘awapiga mkwara’ wafugaji
Habari Mchanganyiko

Mrisho Gambo ‘awapiga mkwara’ wafugaji

Makundi ya Ng'ombe yaliyokutwa katika Poro Tengefu la Loliondo
Spread the love

MKUU wa Mkoa Arusha, Mrisho Gambo amesema mwananchi yeyote atakayeshindwa kutoa ushirikiano wa kujua idadi ya mifugo aliyo nayo atatiwa nguvuni, anaandika Mwandishi Wetu.

Akizungumza wakati wa kuzindua kazi ya ukusanya takwimu iliyofanyika kwenye kata ya Olbalbald, alisema serikali imeamua kufanya sensa ili kujua idadi sahihi itakayoweza kuwasaidia wananchi wa eneo hilo kupata misaada.

“Kujua idadi ya mifugo itatusaidia serikali kujua hata kama tunaleta chanjo za mifugo basi tujue ni idadi gani na pia kujua mifugo iliyo ni ya eneo hilo au la,” alisema.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Baraza la Wafugaji, Edward Maura, alisema kupitia ukusanyaji wa takwimu ya idadi ya watu na mifugo kwenye eneo hilo, litaweza kusaidia kutoa dira ya maendeleo hasa katika kubainisha maeneo pamoja na matumizi yake.

Amesema eneo hilo linakabiliwa na changamoto nyingi ikiwamo uhaba wa maji, barabara na huduma za kijamii kwa hiyo amesema kujua idadi halisi ya watu itawezesha kutengeneza fursa za kimaisha na kimaendeleo ya wananchi pamoja na serikali.

Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Takwimu, Jocye Saul, alisema ukusanyaji wa sensa umekuwa shirikishi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Songwe awafunda trafki kuzingatia uadilifu

Spread the loveASKARI wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Songwe wametakiwa kuendelea...

Habari Mchanganyiko

Mchimba madini jela maisha kwa kubaka, alihonga Sh 500

Spread the loveMahakama ya wilaya ya Songwe imemtia hatiani na kumhukumu kifungo...

Habari Mchanganyiko

Mlima wa Moto wazindua kongamano la SHILO kumuenzi Rwakatare

Spread the loveKANISA la Mlima wa Moto Mikocheni jijini Dar es Salaam,...

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

error: Content is protected !!