Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mradi wa kuuvuruga Ukawa waiva
Habari za SiasaTangulizi

Mradi wa kuuvuruga Ukawa waiva

Spread the love

MBUNGE wa Kaliua, Magdalena Sakaya, ametoa mwaliko kwa wabunge wote wa Chama Cha Mapinduzi, kuhudhuria tafrija na sherehe kubwa ya kuapishwa wabunge saba walioteuliwa na anayejiita, “mwenyekiti wa CUF,” Ibrahim Lipumba.

Mwandishi wetu kutoka Dodoma anasema, wa mujibu wa mwaliko huo, uliowasilishwa kwenye kikao cha wabunge wa CCM, kilichofanyika jioni ya leo.

Anasema, sherehe hizo zitafanyika kwenye ukumbi wa Didoma Hoteli.
Sakaya ambaye tayari amefukuzwa uanachama wa CUF, lakini akabaki kwenye chama hicho kwa maguvu ya serikali, amenukuliwa akimuahidi Spika wa Bunge, kuwa wabunge wake hao watafanya kazi bega kwa bega na uongozi wake.

Aidha, katika hatua nyingine, magari kadhaa yaliyobeba wafuasi wa Lipumba yameonekana maeneo ya Dodoma ili kuhudhuria kuapishwa kwa wabunge hao wasaliti.

Naye Lipumba ameonekana mjini hapa kuhudhuria sherehe hizo. Anatarajiwa kuingia bungeni kesho asubuhi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!