Sunday , 2 April 2023
Home Kitengo Michezo Mpinzani wa Simba Klabu Bingwa Afrika kujulikana leo
Michezo

Mpinzani wa Simba Klabu Bingwa Afrika kujulikana leo

Spread the love

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), leo 9 Novemba 2020, linatarajia kupanga droo ya michezo ya awali ya michuano ya Klabu Bingwa na Kombe la Shirikisho Afrika huku mwakilishi pekee kwenye michuano kutoka nchini Tanzania ni klabu za Simba mara baada ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa msimu wa 2019/20. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Droo hiyo itapangwa hii leo kwenye makao makuu ya shirikisho hilo yaliopo Cairo, nchini Misri majira ya kwa msimu mpya wa mashindano 2020/21.

Klabu ya Simba itaanza mbio hizo kwenye hatua ya awali kwa kucheza michezo miwili na wakifanikiwa kuvuka hapo itaingia moja kwa moja kwenye hatua ya makundi ya michuano hiyo kama walivyofanya kwenye msimu wa 2018/19.

Sambamba na droo hiyo, pia Caf watatangaza tarehe ya kuchezwa kwa mechi hizo ambapo zitakuwa kwenye mtindo wa nyumbani na ugenini licha baadhi ya timu kutoanzia kwenye hatua hiyo.

Timu ambazo hazitoshiriki kwenye hatua hiyo ya awali ni Al Ahly na Zamalek za Misri, AS Vital Club na TP Mazembe zote kutoka Congo, Waydad AC na Raja Casablanca za nchini Morocco, Esperance (Tunisia), Mamelod Sundowns (Afrika kusini), Horoya na Primerio De Agosto kutoka Angola.

Kikosi cha timu ya Namungo FC

Aidha Shirikisho hilo pia litapanga Droo ya michezo ya kombe la Shirikisho ambapo klabu ya Namungo Fc kutoka Luangwa, Lindi ndio timu pekee itakayoiwakilisha Tanzania kwenye michuano hiyo ambayo ni ya pili kwa ukubwa ndani ya bara la Afrika.

Mara ya mwisho Simba kushiriki michuano ya klabu bingwa ilikuwa msimu wa 2019/20 na ikatolewa kwenye michezo ya awali dhidi ya UD Songo ya kutoka Msumbiji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!