
Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete
MPANGO Rais Jakaya Mrisho Kikwete, kuitaka serikali ya Jamhuri ya India, kutoa msaada wa kujenga Reli jijini Dar es salaam ili kupunguza foleni, umepinga na baadhi ya wananchi na kuita, “usanii wa karne.”
“Ni Kikwete huyuhuyu ambaye miaka 10 iliyopita, aliahidi kujenga reli ya kisiasa ya kutoka Dar es Salaam hadi Rwanda. Ni huyu aliyeahidi ujenzi wa reli kwenda Kenya; na au Kigoma na Mwanza. Lakini mpaka sasa, hakuna kilichofanyika.
“Sasa ikiwa leo, miezi mitatu kabla ya kuondoka Ikulu, ndiyo anakuja na hadithi hii ya reli ya Dar es Salaam? Huu ni usanii wa kupitiliza,” ameeleza Juma Amiri, mkazi wa Tabata jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Waziri Mkuu wa India, Pranad Mukherjee jana mjini New Delhi, Rais Kikwete alisema, anaomba nchi hiyo isaidie ujenzi wa reli hiyo ili kuondoa msongamano wa magari katikati ya jiji.
Hata hivyo, wachambuzi wa mambo ya kisiasa wanakebehi kauli hiyo ya Kikwete kwa madai kuwa, imelenga kuwaghiribu wananchi.
waziri mkuu wa india ni narendra modi. labda ulikuwa unamaanisha rais wa india. halafu taasisi makini kama mwanahalisi stori ina source moja tena mtu wa mtaani! sina maana watu wa mataani sio chanzo cha habari, nilidhani huo usanii ambao wananchi wanapinga ungetiliwa mashiko kwa facts. halafu kwani rais akiweka mipango muda wake ukiwa unayoyoma ni usanii? swali la mwisho kwa mhariri na mwandishi wa stori hii ni kwamba rais ni mtu na sio taasisi? akiwa anamaliza muda lazima awe amamemaliza mambo yake na kusubiri mwingine aje na vyake aanze si ndio maana! uandishi makini kweeeli kweeeeli